• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Bilioni 2.9 Yatolewa kwa wanufaika wa mikopo ya Asilimia 10% ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

Tarehe iliyowekwa: March 7th, 2023

Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kupitia Idara ya Maendeleo ya Jamii leo Machi 7, 2023 wamefanya hafla ya kukabidhi mikopo kwa vikundi vya wanawake, Vijana na watu wenye ulemavu ambapo shilingi bilioni 2.9 zimetolewa ikiwa ni fedha kwa ajili mkopo wa asilimia 10% ya mapato ya ndani ya Halmashauri kwa wanufaika hao.

Aidha Hafla hiyo iliyofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam iliweza kuhudhuriwa na Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Wakuu wa Idara, Wadau wa maendeleo kutoka Bank ya CRDB, NMB, DCB, wajasiriamali wanaonufaika na mikopo ya asilimia 10% pamoja na wananchi wengine wa Jiji la Dar es Salaam.

Akizungumza katika hafla iyo DC Mpogolo amesema “Niwaombe sana wanufaika wa mikopo hii muwe na nidhamu ya marejesho ya fedha hizi kwani Mheshimiwa Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan anatambua uwepo wa makundi haya ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu na ndio maana katika kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Mheshimiwa Rais ameweza kuelekeza Halmashauri zote zitoe mikopo kwa makundi haya pia ameruhusu Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kutoka mkopo hadi bilioni 2.9 lengo likiwa ni kuhakikisha wananchi wanajiajiri wenyewe na wanajikwamua kiuchumi hivyo niwaombe mkipewa mikopo hii mhakikishe mnarejesha fedha hizo kwa wakati ili wengine waweze kupata kwani wahitaji bado ni wengi.”

Sambamba na hilo Mhe.Mpogolo ameeleza kuwa japo vikundi hivi vinapata mikopo na vimejiajiri ila Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam pamoja na timu yake waweze kuwatafutia masoko wananchi hawa wanaopokea mikopo ya asilimia 10%hivyo amewaombaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kupitia idara yake ya maendeleo ya Jamii wanaandaa Soko angalau mara mbili kwa mwaka kwaajili ya kusaidia vikundi hivi.

Kwa upande mwingine Mhe. Mpogolo amewahakikishia Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam pamoja na Mkurugenzi wa Halmsahauri ya Jiji la Dar es Salaam kuwa atashirikiana nao bega kwa bega kuhakikisha wanufaika wa mikopo wanarejesha kwa wakati na kwa wale watakao kaidi watawajibishwa kulingana na kanuni za Kisheria.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Eng. Amani Mafuru ameeleza kuwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kupitia Idara ya Maendeleo ya Jamii inaendelea kutekeleza jukumu la kutenga na kutoa mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu ikiwa ni fedha kutoka mapato ya ndani ambapo hadi kufikia Juni 2022 takribani shilingi bilion 23.4 ziliweza kutolewa kwa vikundi 1963 vyenye wanufaika elfu 19.8 ambapo shilingi bilioni 19.9 zikiwa ni fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri huku shilingi bilioni 5.5 zikiwa ni fedha kutoka katika marejesho ya mikopo hiyo.

Akiendelea kutoa taarifa katika hafla hiyo Eng.Mafuru amesema “kuanzia mwezi Julai 2023 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imeanza kutoa mikopo kwa kuzingatia mfumo wa kielektronic (Ten Percent Loan Management Infomation System) ulioanzishwa na Serikali kuu kwa lengo la kurahisisha usimamizi na ufuatiliaji wa mikopo hiyo hivyo kupitia mfumo huu Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imeweza kusajili takribani vikundi 1870 na imepokea jumla ya maombi ya mkopo kwa vikundi 458 vyenye thamani ya shilingi bilioni 33 ambapo baada ya uhakiki Halmashauri imepanga kutoa mikopo hiyo kwa awamu kupitia fedha za marejesho kutoka kwenye mikopo ya vikundi vingine.”

Sambamba na hilo Eng. Mafuru ameeleza kuwa “lkiwa ni awamu ya Kwanza ya mwaka wa fedha 2022/2023 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam inatoa mikopo kwa vikundi 76 vyenye wanavikundi 360 ambapo vikundi 27 vinatoka Jimbo la Ilala, vikundi 23 kutoka Jimbo la Ukonga huku vikundi 26 vikitoka Jimbo la Segerea ambapo vikundi hivyo vitapewa mkopo kulingana na mgawanyo wa asilimia 4% kwa Wanawake, asilimia 4% kwa vijana na asilimia 2% kwa watu wenye ulemavu kwani vikundi hivi vimeshapata mafunzo na kusaini mikataba tayari kwa kuwekewa hela hizo."

Akitoa Shukurani zake za dhati kwa niaba ys wanavikundi wengine waliopokea hundi za mfano Deogratius Davidi kutoka kikundi cha Good Hope ameweza kumshukuru Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan kwa utoaji wa mikopo bila kusahau juhudi za Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kupitia Idara ya Maendeleo ya Jamii kwa kuweza kuandaa mafunzo na pia kutoa ushauri kwa vikundi hivyo kwani hii imeweza kupunguza wimbi la ukosekanaji wa ajira kwa vijana hivyo wameahidi kuzitumia fedha hizo kwa umakini na kurejesha marejesho kwa wakati ili wengine waweze kunufaika.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.