• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

DC Ludigija Ashiriki zoezi la usafi wa mwisho wa Mwezi Julai

Tarehe iliyowekwa: June 25th, 2022

Katika kutekeleza Kampeni ya Usafi iliyozinduliwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ya ‘Pendezesha Safisha Dar es Salaam’ Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam leo tarehe 25 Juni, 2022 wamefanya usafi katika kata ya Jangwani ikiwa ni sehemu ya kuendeleza kampeni ya Safisha Pendezesha Dar es Salaam ambapo usafi huo hufanywa kila Jumamosi ya Mwisho wa Mwezi.

Zoezi hilo la usafi lililoongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mheshimiwa Ng’wilabuzu Ludigija liliweza kuhudhuriwa na watu mbalimbali akiwemo Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Diwani wa Kata ya Jangwani, Jeshi la Zimamoto, Watendaji kutoka Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Asasi mbalimbali ikiwemo ‘Juza Waste Pickere Initiative’ Taasisi ya kutokemeza kifua kikuu, pamoja na wananchi wa Kata ya Jangwani wakiongozwa na vijana walioathiriwa na madawa ya kulevya ambao kwasasa wamesaidiwa na Juza Waste Pickers Initiative ambao hujishughulisha na uokotaji wa taka ikiwa ni sehemu ya utunzaji wa mazingira.

Akizungumza katika zoezi hilo Mheshimiwa Ludigija amewata Wananchi kushiriki usafi kama desturi yao na sio kusubiri mpaka mwisho wa mwezi ufike ili kuweka mazingira safi na kuhakikisha Jiji la Dar es Salaam linapendeza na kuwa safi, "Tuhakikishe kwamba usafi ni jambo la kwanza katika Wilaya yetu na ukilinganisha kwamba sisi ni Jiji Lazima tuendane na hadhi ya Jiji letu hivyo nipende kutoa wito kwa Mtendaji wa Kata ya Jangwani kuhakikish kua anashirikiana na  viongozi pamoja na wadau  wengine kuwatumia vijana wa kata hii kuokota taka Lengo likiwa ni kupendezesha Jiji na kutekeza kampeni yetu ya Safisha Pendezesha Dar es Salaam hivyo tuufanye usafi kama desturi yetu na tusisubiri hadi mwisho wa mwezi ufike."

Sambamba na hilo Mheshimiwa Ludigija ameweza kuzindua Asasi ya utunzaji wa Mazingira maarufu kama ‘Juza Waste Pickers Initiative’ ambayo ilianza mwaka 2012 kama kikundi kidogo cha waokota taka wakisaidiwa na vijana walioathiriwa na madawa ya kulevya ambapo hadi kufikia Aprili, 2022 Juza Waste Pickers Initiative kusajiliwa rasmi na kua Asasi ya Utunzaji wa Mazingira, aidha Asasi hiyo imekua ikishirikiana na vijana hao kwa ukaribu zaidi lengo likiwa ni kuwawezesha vijana kiuchumi na pia kuwafanya waondokane na matumizi ya madawa ya kulevya na kurudi katika hali zao za kawaida."Amesema Mheshimiwa Ludigija.

"Niwapongeze kwa jambo hili zuri la kuwasaidia vijana wetu kuondokana na wimbi la uvutaji madawa ya kulevya na kuamua kuwaajiri katika kazi ya kutunza mazingira ambapo hadi sasa wamekua wakijali afya zao hivyo kuamua kutoa bima za afya  kwa vijana 30 Lengo likiwa ni kuhakikisha wanaimarisha afya za vijana hao, hivyo niwakaribishe wadau wengine watakaowiwa katika hili lengo likiwa ni kumuunga mkono Mheshimowa Raisi katika kuimarisha sekta ya Afya.

Kwa upande mwingine Mheshimiwa Ludigija amewasisitiza wananchi kushiriki vyema katika zoezi la Anuani za Makazi ambapo amewaagiza kuhakikisha wanaweka namba kwenye nyumba zao pamoja na vibao vya mitaa  lengo likiwa ni kurahisisha mawasiliano majanga yanapotokea na pia kuimarisha biashara zao lakini pia zoezi hilo la Anuani za Makazi litarahisisha zoezi la Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022 inayotarajiwa kufanyika  mwezi wa Nane mawaka huu.

"Natoa Wito kwa viongozi wa Kata wakiongozwa na Madiwani husika kuhakikisha wanasimamia vizuri zoezi la Anuani za makazi kwa kuhakikisha Mitaa yote inakua na vibao pamoja na nyumba zote kua na Namba hivyo niwaombe wananchi kushiriki vizuri kwa kuhakikisha nyumba zao zina namba.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.