• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

DC Mpogolo alipongeza Jiji la DSM kwa kuboresha Sekta ya Afya

Tarehe iliyowekwa: June 28th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Mpogolo ameipongeza Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa kuendelea kuboresha huduma za afya kwa wananchi. Pongezi hizo amezitoa leo Juni 28, 2024 wakati wa Hafla ya ugawaji vifaa tiba kwa Idara ya Afya iliyofanyika katika ukumbi wa Arnatoglou Jijini humo.

Akikabidhi vifaa hivyo Mhe Mpogolo amesema “Napenda kuipongeza Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa ukusanyaji wa mapato zaidi ya bilioni 100 ambapo wameweza kuvuka lengo la kukusanya bilioni 89 kwani kupitia fedha hizi wameweza kununua vifaa tiba vya shiingi Bilioni 1.6 huku zaidi ya milioni miatatu zikitumika kununua vifaa vya TEHAMA na Milioni 11 zikitumika kukata bima za iCHF kwa watoa huduma za afya ngazi ya Jamii hivyo kutokana na vifaa hivi huduma za afya zinaendelea kuboreshwa katika Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam na hii inaonesha jinsi gani Jiji la Dar es Salaam linatimiza adhma ya Mheshimiwa Rais WaJamhuri  ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha huduma za afya zinaboreshwa na zinawafikia wananchi kwa wakati.”

Sambamba na hilo, Mhe.Mpogolo aliweza kukabidhi vyeti vya mafunzo kwa timu za usimamizi vituoni (HMT’S 164) pamoja na bima za afya 277 kwa watoa huduma ngazi ya jamii huku akiwataka watoa huduma za jamii ngazi ya afya kuwa waadilifu kwa kuhakikisha wanazingatia utoaji wa huduma bora kwa wananchi pamoja na kutoa wito kwa viongozi waliopatiwa vyeti vya mafunzo kuhakikisha wanajali wananchi wanaowahudumia bila kusahau kubainisha changamoto za afya zilizopo ngazi ya jamii ili zipatiwe ufumbuzi.

Kwa upande wake Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mhe. Omary Kumbilamoto  ameeleza kuwa Jiji la Dar es Salaam limepata bahati ya kupata fedha nyingi kutoka Serikali Kuu ambazo zinatumika kwenye Miradi ya Afya , Elimu na kuboresha miundombinu ya afya hivyo kutokana na ukusanyaji mkubwa wa mapato Jiji la Dar es Salaam limeweza kununua vifaa tiba ili kuhakikisha huduma za afya katika Jiji hilo zinaimarika kwa kasi.

Naye Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam Ndg. Jomaary Satura ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuendelea kuboresha sekta ya afya huku alieleza kuwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kupitia mapato yake ya ndani inaenda kutekeleza ujenzi wa hospitali kubwa tatu zitakazoenda kupunguza changamoto ya msongamano wa wagonjwa pamoja na kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi na kwa wakati.

Awali akitoa taarifa kwa Mkuu wa Wilaya, Mganga Mkuu wa Jiji la Dar es Salaam Dkt. Zaituni Hamza ameeleza kuwa “Katika kuendelea kutoa huduma bora za afya kwa jamii, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kupitia Idara ya Afya ilipanga kununua vifaa tiba mbalimbali kwa mwaka wa fedha 2023/2024 vya jumla ya shilingi bilioni 1.6 ikiwa ni fedha kutoka mapato ya ndani ya Halmashauri pamoja na Serikali kuu ambapo leo tumeweza kukabidhiwa Ultra Sound 15 pamoja na vifaa vya TEHAMA ambavyo vinaenda kuleta mabadiliko katika sekta afya kwenye Jiji letu hivyo tunaahidi kufanya kazi kwa ufanisi na weledi ili wananchi waweze kupata huduma bora kwa wakati.”




Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.