• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

DC Mpogolo asikiliza kero za Wananchi wa Kata za Mnyamani na Vingunguti

Tarehe iliyowekwa: October 18th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Mpogolo leo Oktoba 18, 2023 amefanya ziara ya kusikiliza na kutatua kero za Wananchi wa Kata ya Vingunguti pamoja naKata ya Mnyamani ikiwa ni utaratibu wake wa kuwafikia wananchi kusikiliza na kutatua kero zao.

Akiwa katika kusikiliza kero za wananchi wa Kata ya Vingunguti eneo la Mabuchani Mhe. Mpogolo amesema amebaini kero kubwa kutoka kwa wananchi wa Kata ya Vingunguti ni kukosekana kwa wataalamu wa ngozi hivyo kufanya watu wa mabucha kutupa ngozi hizo, ukosefu wa Dawa katika kituo cha Afya Buguruni, pamoja na ubovu wa huduma za kampuni za uzoaji taka.

Hata hivyo Mhe. Mpogolo amewataka Viongozi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam hususani Mkuu wa Divisheni ya Mifugo na Uvuvi kuhakikisha anatafuta wataalamu wa ngozi ili kuona namna gani ya kuboresha huduma ya ngozi pia amemtaka ahakikishe eneo la nje la machinjio linaboreshwa kuelekea katika msimu wa mvua.

“Niwaombe Viongozi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kuandaa kikao na wataalamu wa ngozi ili tuweze kuboresha huduma za ngozi kwani ngozi ina thamani kubwa na itatuingizia mapato hivyo na mimi nitashirikiana na Mstahiki Meya kutafuta wataalamu hao tuone namna gani watatuelekeza kuhusu uboreshaji wa ngozi hizo za wanyama pia tuhakikishe tunaboresha zaidi huduma katika machinjio yetu lengo likiwa ni kuzuia upotevu wa mapato yetu kwani Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ametenga fedha kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya Elimu, Afya na Barabara hivyo mapato hayo yatasaidia katika utekelezaji wa miradi hiyo ya Maendeleo.” Amesema Mhe. Mpogolo

Kwa upande Mwingine Mhe. Mpogolo ameweza kusikiliza kero za Wananchi wa Mnyamani na kumuelekeza Mganga Mkuu wa Jiji la Dar es Salaam kuhakikisha huduma za afya katika kituo cha afya Buguruni zinaboreshwa hususani eneo la huduma kwa wateja kwani inaonekana wahudumu wa kituo hicho hawana huduma nzuri kwa wagonjwa wao.

Sambamba na hilo, Mhe. Mpogolo amewataka Wananchi wa Kata ya Mnyamani pamoja na vingunguti kutoa ada za taka na pia kuwa wavumilivu kwani suala la mkandarasi anaezoa taka maeneo hayo litafanyiwa kazi huku akiwataka Wananchi hao kufika ofisini kwake pindi wanapokua na malalamiko.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam aliweza kumuhakikishia Mkuu wa Wilaya kutekeleza yote aliyowaagiza ili kuboresha huduma na kuzuia upotevu wa mapato ya Halmashauri.

Mwisho wananchi na viongozi wa Kata za Mnyamani na Vingunguti wamepongeza ziara ya Mkuu wa Wilaya kwa kuwakumbuka katika kusikiliza kero zao na kumuhakikishia kutekeleza yote aliyoyaagiza. Ziara hii ni endelevu kwa kata zote 36 za Ilala.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.