• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

DSM-Hamburg Partnership wagawa Vifaa vya kujikinga na UVIKO 19 kwa Watoto wenye mahitaji Maalumu

Tarehe iliyowekwa: October 12th, 2021

Na: Rosetha Gange

Wakati wataalamu wa afya dunia wakiendelea kuumiza vichwa juu ya tiba ya kulimaliza kabisa janga la UVIKO 19, hapa kwetu Tanzania Serikali kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali zimekuwa zikiungana na wataalamu hao duniani kote katika kupunguza maambukizi ya ugonjwa huo ikiwa ni pamoja na kuhamasisha watu kupata chanjo, kuepuka mikusanyiko isiyo ya lazima, kuvaa barakoa wawapo kwenye mikusanyiko, kutumia vitakasa mikono na kunawa mikono kwa maji tiririka mara kwa mara.

Katika kuunga mkono jitihata zinazofanywa na Serikali ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania,Shirika la Dar es salaam Hamburg Partnership linalomilikiwa na watu wa Ujerumani hapa Tanzania limegawa vifaa vya kujikinga dhidi ya maambukizi ya UVIKO 19 katika shule mbalimbali za watoto wenye mahitaji maalumu katika mkoa la Dar es salaam pamoja na kutoa elimu kwa watoto hao ya namna ya kutumia vifaa hivyo na njia nyingine za kujikinga na virusi vya Uviko 19.

Zoezi la ugawaji wa vifaa hivyo ulianza tarehe 4/10 na kumalizika 12/10/2021. Vifaa vilivyogawiwa ni Pamoja na stendi za chuma kwa ajili ya kuwekea ndoo za maji, ndoo za kutunzia maji na bomba zake, sabuni za maji za kunawia mikono pamoja na barakoa.

Akikabidhi vifaa hivyo Dr. Sylivia Ruambo ambaye ndiye Mratibu wa zoezi hilo amesema “Kama tunavyojua janga hili la UVIKO 19 lipo na tunapaswa kujikinga nalo sababu halichagui mtu mzima wala mlemavu.Tumeamua kuwasaidia Watoto wenye ulemavu kwa namna ya pekee kwa sababu changamoto wanazozipata wengine sababu ya ugonjwa huu na wao wanazipata lakini wao kutokana na hali walizonazo changamoto hizo huwa kubwa zaidi. Hivyo njia za kuwakinga kirahisi ni kuwawekea mashine za kunawia mikono karibu ili kuwarahisishia walimu na walezi wao waweze kuwasaidia kirahisi”  

Shule zilizokabidhiwa msaada wa vifaa hivyo ni Pamoja na Shule ya Sekondari Pugu, Shule ya msingi Mzambarauni, Shule ya msingi Buguruni Viziwi, shule ya Msingi Msimbazi Mseto,Shule ya sekondari Benjamini Mkapa,Shule ya msingi Uhuru mchanganyiko, Shule ya Sekondari ya wasichana Jangwani,Shule ya msingi Mtoni Maalumu, Shule ya msingi Sinza maalumu na Shule ya msingi Msasani.

Akiongea kwa niaba ya Mkurugenzi wa Jiji la Dar es salaam, Afisa Elimu Maalumu wa Jiji Ndg.Swalehe Msechu ameishukuru Taasisi hiyo kwa kuwakumbuka watoto wenye changamoto mbalimbali kwani katika jamii mara nyingi kundi hili huwa linasahaulika sana. Hivyo kuwapa elimu ya kujikinga dhidi ya maambukizi ya UVIKO 19 kutawaepusha wao wenyewe na familia zao katika hatari ya kupata maradhi hayo.Pia ameahidi kusimamia utunzaji wa vifaa vyote vilivyokabidhiwa ili viweze kutumika katika matumizi sahihi yaliyokusudiwa.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.