• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Hafla ya kutia saini Mkataba wa Ushirikiano wa majiji ya Hamburg na Dar es Salaam

Tarehe iliyowekwa: November 14th, 2017

DAR ES SALAAM na Hamburg zimefungua ukurasa mpya wa uhusiano wao wa Miji Dada kwa kusaini mkataba mpya wa uhusiano kati yao. Mkataba huo umesainiwa Novemba 14, mwaka huu katika Jiji la Hamburg na Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita na Mstahiki Meya wa Jiji la Hamburg, Olaf Scholz, ukishuhudiwa na Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Sipora Liana, watendaji wakuu wa mamlaka ya Jiji la Hamburg na taasisi mbalimbali za Serikali katika Jiji hilo, wawakilishi wa asasi za kiraia na baadhi ya Watanzania wanaoishi Hamburg. 

Mkataba wa awali wa uhusiano huo ulitiwa saini mwaka 2010 na Adam Kimbisa na Ole Van Beust waliokuwa mameya wa majiji hayo katika kipindi hicho.

Mstahiki Meya na Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam waliwasili katika Jiji la Hamburg kwa ziara ya kikazi na kusaini mkataba huo wakitokea katika mji wa Bonn ambako walishiriki katika mkutano wa mabadiliko ya tabia nchi ulioandaliwa na taasisi ya Engagement Global ya Ujerumani kwa miji washirika wa Ujerumani. 

Viongozi hao wawili wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam wakiwa mjini Bonn walishiriki pia katika mkutano wa mameya na magavana ambao ulikuwa sehemu ya mkutano ulioandaliwa na Umoja wa Mataifa wa COP23 ambao umefanyika sambamba na mkutano ulioandaliwa na Engagement Global.

Kabla ya kusainiwa kwa mkataba huo, vikao vya wataalam mbalimbali wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Engagement Global, miji wa shirika na wataalam wa Wizara ya Maendeleo ya Miji na Makazi wa Jiji la Hamburg, vilifanyika mjini Bonn na Hamburg kwa usimamizi wa Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam na Mtendaji Mkuu wa Jiji la Hamburg,Wolfgang Schmidtz, kubaini maeneo mengi zaidi ya ushirikiano kati ya miji hiyo, wahusika na miradi mipya inayoweza kutekelezwa kwa ufanisi na kwa manufaa ya wananchi kupitia uhusiano huo.

Pande hizo mbili, hasa kwa kuzingatia matakwa ya Dar es Salaam, zimekubaliana kushirikiana katika maeneo mabadiliko ya tabia nchi ikiwa ni pamoja na kutoa elimu kwa umma kuhusu namna ya kukabiliana na mabadiliko hayo, upangaji wa miji, uboreshaji wa huduma za usafiri wa umma na shughuli za kukuza utalii katika Jiji la Dar es Salaam.

Baada ya kusainiwa kwa mkataba huo, viongozi hao wa Jiji la Dar es Salaam walikutana na Bodi ya Ushauri ya Jiji la Hamburg na kisha kuwa na mkutano mwingine na wadau wa uhusiano huo wakiwemo Watanzania wanaoishi Hamburg ambao wajumbe wote kwa ujumla walisisitiza kila upande ufanye jitihada za dhati za kuimarisha ushirikiano huo kwa kuacha urasimu, kutojihusisha na vitendo vya rushwa, kuwa wawajibikaji zaidi na kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano kuwa na Tanzania ya viwanda.

Hii ni safari ya kwanza ya kikazi nje ya nchi kwa Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita na Mkurugenzi wa Jiji hilo, Sipora Liana, kusafiri pamoja na kurejea nchini wakiwa wamefanikiwa katika kutimiza malengo ya safari yao mjini Bonn na Hamburg.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.