• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Jiji la DSM laadhimisha Siku ya Lishe Kitaifa

Tarehe iliyowekwa: October 30th, 2023

Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa kushirikiana na Shule za Msingi Kisutu na Mtendeni leo tarehe 30, Oktoba, 2023 wamefanya hafla ya Maadhimisho ya Siku ya Lishe Kitaifa yaliyofanyika katika Shule ya Msingi Kisutu, yenye kauli mbiu inayosema "Lishe Bora kwa Vijana Bqlehe, Chachu ya Mafanikio yao"

Akiongea katika Maadhimisho hayo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Afisa Elimu Msingi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Bw. Hossein Mghewa amesema "Nia ya Siku ya Lishe ni kuelimisha umma kuhusu lishe na utapiamlo kwa Tifa letu hasa kwa watoto na vijana, kwani vijana ndio nguvu kazi ya Taifa letu. Hivyo nawasihi vijana kuacha kula vyakula visivyofaa kwa sababu havina madini na vitamini zinazofaa katika ukuaji zaidi husababisha kupata balehe za mapema hivyo tupendelee kula mbogamboga na matunda, kwa sababu vijana mlio kwenye balehe mnahitaji lishe bora."

Sambamba na hilo Bw. Mghewa ametoa shukrani zake kwa waalimu, wanafunzi na wote walioshiriki katika maandalizi ya Maadhimisho ya siku ya lishe kitaifa na kuwaomba walimu wote wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kuwa na vikundi (clubs) za kuhamasisha lishe bora katika shule zote za msingi.

Aidha, mratibu wa Lishe wa Halmashauri ya Jiji la DSM Bi. Flora Mgimba amesema "Lishe ni jambo la msingi katika makuzi ya mtoto na kijana katika taifa letu ndio maana Serikali yetu iliona umuhimu wa kua na maadhimisho ya siku ya lishe kwa sababu vijana ndio taifa la kesho na vijana ndio nguvu kazi ya Taifa, na tunahitaji vijana wenye Afya njema katika kulijenga taifa letu, lishe Bora inaendana na mazoezi hivyo nawaasa hii elimu mnayoipata mkaipeleke kwa familia zenu na jamii inayowazunguka."

Akiongea kwa niaba ya walimu na wanafunzi, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kisutu Mwl. Elizabeth Massawe amemshukuru mgeni rasmi kwa kushiriki pamoja nao kwani elimu na kuahidi kuendelea kutoa Elimu ya lishe bora kwa wanafunzi kwa njia ya masomo, nyimbo na maigizo.

Maadhimisho ya siku ya lishe yalianza rasmi Julai 2020 ambapo huadhimishwa kila tarehe 30 Oktoba.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.