• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Jiji la DSM lapitisha Mpango na Bajeti ya Shilingi Bilioni 193.8 kwa mwaka wa fedha 2022/2023

Tarehe iliyowekwa: February 8th, 2022

Na: Hashim Jumbe

BARAZA la Madiwani Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, leo Tarehe 08 Februari, 2022 limefanya Mkutano Maalum wa Mapitio na Bajeti ya mwaka 2021/2022 kwa kipindi cha nusu mwaka (Julai-Desemba, 2021) na kufanya Makisio ya Mpango na Bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023 wenye Jumla ya Shilingi Bilioni 193.8, ambapo kati ya fedha hizo Shilingi Bilioni 73.9 sawa na 38.1% ya Bajeti yote ni kutoka kwenye vyanzo vya mapato ya ndani ya Halmashauri na Shilingi Bilioni 119.9 sawa na 61.85% ya Bajeti ni fedha za Ruzuku kutoka Serikali Kuu ambazo ni kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo na Matumizi ya kawaida.

Aidha, kikao hicho kilichofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa Arnatouglou na kuongozwa na Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mhe. Omary Kumbilamoto, kilipokea, kikajadili na kisha kupitisha Mpango na Bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023 ambapo Bajeti ya Mapato ya ndani ya Halmashauri ya mwaka  wa fedha 2022/2023 imeongezeka kwa 16% ukilinganisha na Bajeti ya Shilingi Bilioni 62 ya mwaka 2021/2022, hii imetokana na mikakati bora iliyowekwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwenye ukusanyaji wa mapato.

Katika kuandaa Mpango na Bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imezingatia Muongozo wa uandaaji wa Bajeti uliotolewa na Hazina Mwezi Februari, 2021, Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya Mwaka 2020, Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, aliyoitoa Bungeni.

Sambamba na hayo, lakini pia uandaaji wa Mpango na Bajeti umezingatia Sheria ya Bajeti Na. 11 ya mwaka 2015 sura 439 pamoja na kanuni zake, Mkakati wa Taifa wa Mapambano dhidi ya rushwa, Malengo ya Mellania (SDGs 2030) Mpango Mkakati wa Halmashauri, Maoni ya wadau mbalimbali wa Halmashauri ambao wameshiriki katika maandalizi ya bajeti hii kuanzia ngazi ya Mtaa, Kata, Idara hadi Halmashauri kwa ujumla kwa kutumia mfumo wa Frursa na Vikwazo (O & OD iliyoboreshwa)

Aidha, katika makisio ya Mpango na Bajeti ya mwaka 2022/2023 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imejiwekea vipaumbele vyake pamoja na mikakati kumi na nne (14) itakayosaidia kufanikisha ukusanyaji wa mapato ya ndani ya Halmashauri ili iweze kutekeleza Mpango na Bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023 kwa asilimia 100

Makisio ya Mapato ya Ndani ya Halmashauri kwa mwaka 2022/2023

Akisoma taarifa kuhusu makisio ya mpango na bajeti ya mwaka 2022/2023 mbele ya Baraza la Madiwani, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Ndugu Jumanne Shauri, alisema "Kwa mwaka wa fedha 2022/2023 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imepanga kukusanya  Shilingi Bilioni 73.9 kutoka kwenye vyanzo vyake vya ndani"

Matumizi ya Mapato ya ndani ya Halmashauri kwa mwaka 2022/2023

"Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa mwaka wa fedha 2022/2023 kwenye Mapato yake ya Ndani inatarajia kutumia fedha kiasi cha Shilingi Bilioni 73.9 katika mchanganuo ufuatao; Matumizi Mengineyo Shilingi Bilioni 22.04 sawa na 29.8% ya Bajeti, Mishahara Shilingi Bilioni 1.26 sawa na 1.7% ya Bajeti, Miradi ya Maendeleo Shilingi Bilioni 34.96 sawa na 47.26% ya Bajeti na Vyanzo Fungiwa Shilingi Bilioni 15.69 sawa na 21.21% ya Bajeti" Mkurugenzi Shauri

Makisio ya fedha za Ruzuku kutoka Serikali Kuu

Ruzuku ya Shilingi Bilioni 119.9 kutoka Serikali Kuu imegawanywa katika maeneo mawili ambayo ni Matumizi ya Kawaida na Miradi ya Maendeleo

Mchanganuo wa Matumizi ya kawaida kwa fedha ya Ruzuku

"Kwa mwaka wa fedha 2022/2023 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam inatarajia kutumia Shilingi Bilioni 98.15 ya fedha ya ruzuku sawa na 81.83% kulipa Mishahara na Shilingi Bilioni 2.628 sawa na 1.77% sawa na 1.47% kwa ajili ya Matumizi Mengineyo" alisema Shauri

Mchanganuo wa fedha za Miradi ya Maendeleo kwa fedha ya Ruzuku

Katika kipindi kijacho cha 2022/2023 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imepanga kutumia Shilingi Bilioni 19.99 kutekeleza Miradi ya Maendeleo ambayo ni sawa na 16.66%.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.