• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Jiji la DSM latoa mafunzo kwa Watumishi wanaotaraji kustaafu

Tarehe iliyowekwa: February 8th, 2023

Halmashauri ya Jijj la Dar es Salaam kupitia Idara ya Utawala na Utumishi leo Februari 8,2023 wameandaa Semina na kutoa Mafunzo kwa watumishi wanaokaribia kustaafu hivi karibuni, Mafunzo hayo yaliyofanyika katika Ukumbi wa Karimjee Jijini Dar es Salaam yaliwajumuisha Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Afis Utumishi wa Jiji la Dar es Salaam, Watumishi ambao ni wakufunzi kutoka chuo cha Utumishi wa Umma, watumishi kutoka mfuko wa hifadhi ya jamii 'PSSF' pamoja na watumishi kutoka bank ya CRDB.

Akifungua mafunzo hayo Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es-Salaam Bi. Tabu Shaibu amesema, baadhi ya watumishi wamekuwa wanahangaika na kulalama kwa changamoto ya ugumu wa maisha mara baada ya muda wao wa utumishi kuisha na kurudi uraiani kuanza maisha mengine nje na kazi ya utumishi wa Umma, ambapo waliowengi hushindwa kuwa na mipango madhubuti ya baadaye.

Akiendelea kuongea katika mafunzo hayo Bi. Tabu Shaibu ameeleza kuwa, kila mtumishi anawajibu wa kuonesha mchango wake mkubwa muda wote hata baada kutoka kazini, jambo linalotoa taswira nzuri na kuonesha mchango mkubwa kwa jamii, kufanya hivyo kutasababisha kuepuka changamoto zinazoweza kujitokeza wakati wa kustaafu "Tunachokitaka ni kuwa na mchango mkubwa wa wastaafu katika Halmashauri yetu kwani wengi wanaonekana kuogopa kuanza maisha ya uraiani hivyo ni matumaini yangu mafunzo haya yatakua ni njia ya mafanikio kwa watumishi hao wanaoelekea kustaafu"

Aidha, kwa upande wake Afisa utumishi wa Halmashauri ya Jiji la Dares-Salaam, Bi. Benadeta Mwaikambo amebainisha jumla ya watumishi 91 wanatarajia kustaafu kuanzia mwezi Januari mpaka mwezi Desemba mwaka huu akiongeza kuwa kushindwa kuanzisha miradi ya kujikimu kwa watumishi wanapostaafu kuwa ni changamoto kubwa inayowakabili waliowengi baada ya utumishi wao hivyo ofisi ya utumishi ikaamua kuanziisha mafunzo ya kuwaweka tayari wastaafu hao pindi wanapomaliza kuutumikia Umma nakuona maisha mengine kama maisha ya Utumishi.

“Sisi kama Ofisi ya Utumishi tumeona ni vyema kuanzisha mafunzo haya kwani tumebaini kuwa watumishi wengi wa Umma pindi wanapostaafu wanakosa muelekeo wa maisha kwa kuwa walishazoea maisha ya Utumishi hivyo ni katumaini yangu kwamba mafunzo haya yatawapa mwanga wa kuweza kupambana baada ya maisha ya Utumishi wa Umma hii ndo sababu tumewaletea wakufunzi kutoka chuo cha Utumishi wa Umma pamoja na watumishi kutoka mfuko wa hifadhi ya jamii PSSF ili waweze kupata elimu itakao wafanya wajiandae vyema na maisha ya ustaafu na kuyaona ni kama maisha ya Utumishi wa Umma.”

Sambamba na hilo Bi. Mwaikambo ameeleza kuwa zoezi hili lililoanza la utoaji wa mafunzo ni endelevu na kila mwaka watakua wanafanya mafunzo hayo ya kuwaandaa wastaafu kukabiliana na changamoto zitakazowakabili pindi wanapomaliza majukumu yao ya kuutumikia Umma.

Akitoa Shukrani zake kwa Ofisi ya Utumishi kwa niaba ya Watumishi wengine wanaotarajia kustaafu hivi karibuni Bwana Nashon ameeleza kuwa Sisi kama watumishi tunaotarajia kuataafu tumejiandaa vyema kupokea mafunzo haya na tunawahakikishia yote tutakayoelekezwa tutayafuata na kuyafanyia kazi ili yaweze kutuongoza baada ya maisha ya kuutumikia Umma.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.