• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Kamati ya Kudhibiti UKIMWI Halmashauri ya Jiji la DSM yapata mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kupambana na maambukizi ya UKIMWI

Tarehe iliyowekwa: May 2nd, 2023

Katika kutekeleza sera ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kupitia Idara ya Maendeleo ya Jamii Leo Mei 02, 2023 wametoa mafunzo kwa Kamati ya kudhibiti VVU/UKIMWI ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam lengo likiwa ni kuwajengea uwezo wa namna ya kudhibiti maambukizi ya ugonjwa wa UKIMWI katika Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam.

Mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Arnatouglou uliopo Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam yaliweza kuhudhuriwa na madiwani ambao ni wajumbe wa Kamati ya kudhibiti UKIMWI Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ikiongozwa na Naibu Meya wa Jiji, Maafisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam pamoja na viongozi wote wa baraza la watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI (KONGA).

Akifungua Mafunzo hayo Naibu Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Mhe. Ojambi Masaburi ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya kudhibiti UKIMWI amesema “Ni matumaini yangu mafunzo Haya yatawajengea ninyi Kama Kamati ya kudhibiti UKIMWI uwezo juu ya namna ya kudhibiti UKIMWI katika Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwani Nina Imani mtashirikiana na wadau mbalimbali katika kupambana na ugonjwa huo hatarishi na hatimaye kufikia malengo mliyojiwekea.”

Akiwezesha mafunzo hayo maratibu wa VVU/UKIMWI Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam (CHAC) Ndg. Barnabas Kisai ameeleza kuwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wameendelea kutekeleza afua mbalimbali za kudhibiti VVU na UKIMWI kwani Halmashauri kupitia mapato ya ndani imekua ikitenga fedha kiasi cha shilingi milioni 150 kwaajili ya kuhakikisha Jamii inahamashwa zaidi juu ya namna ya kujikinga na ugonjwa wa UKIMWI na pia kuhakikisha wale wote walioadhirika na ugonjwa huo kujitokeza kwa wingi ili kuweza kupata huduma kwa karibu zaidi.

Aidha Ndg. Kisai aliweza kutoa maelezo jumla ya uratibu wa shughuli za VVU/UKIMWI katika Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam huku akiwakumbusha Wajumbe wa Kamati ya kudhibiti UKIMWI wajibu na majukumu yao katika kuhakikisha wana tekeleza afua mbalimbali za kudhibiti ugonjwa wa UKIMWI na pia kuendelea kutoa elimu kwa Wananchi wa Kata zao juu ya namna ya kudhibiti ugonjwa wa UKIMWI. “Japo tunawakumbusha majukumu yenu lakini pia tunawashukuru sana Madiwai wa Kamati yetu ya kudhibiti UKIMWI kwa kupambana kuhakikisha Kamati inaendelea na utekelezaji wa afua mbalimbali za VVU na UKIMWI katika Halmashauri yetu." Ameeleza Ndg. Kisai

Naye Mratibu wa kudhibiti VVU/UKIMWI Sekta ya Afya  Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Dkt. Aisha Zuheri (DACC) ameeleza kuwa “Idadi kubwa ya waadhirika wa ugonjwa wa UKIMWI ni vijana wa kike kuanzia umri wa miaka 15 hadi 24 lakini kutoka na jitihada za kutoa elimu Mara kwa mara katika Kliniki zetu tumeweza kufikia asilimia 102.8 ya kufubaza virusi vya UKIMWI katika Halmashauri yetu.”

Sambamba na hilo Dkt. Aisha ameweza kutoa tofauti kati ya VVU na UKIMWI ambapo ameeleza kuwa VVU ni vimelea vidogo ambayo havionrkani kwa macho huku UKIMWI ikiwa ni mkusanyiko wa magonjwa yanayotokana na kudhoofika kwa nguvu za mwili kujikinga na maradhi hivyo sio kila mwenye VVU ana UKIMWI.

Kwa upande wake mwenyekiti wa baraza la watu wanahis hi na VVU/UKIMWI (KONGA) Bw. Emmanuel Robert Msinga amesema “Napenda kutoa shukrani zangu kwa madiwani wa Kamati ya kudhibiti UKIMWI pamoja na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kupitia Idara ya Maendeleo ya Jamii kwani wamekua na mchango mkubwa sana katika kuhakikisha sisi kama KONGA tunapambana zaidi hadi tumeweza kuanzisha mashamba mbalimbali pamoja na mifugo mbalimbali hii inadhihirisha kuwa sio kila mwathirika wa Ugonjwa wa UKIMWI hawezi kufanya kazi hivyo niwaombe vijana wengine pamoja na watu wengine wenye maambukizi ya ugonjwa wa Uko wasisite kujitokeza na kuungana nasi bila kuogopa kwani sio kila aliyepata maambukizi ndo mwisho wa maisha.”

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.