• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Madiwani Jiji la DSM wafanya uchaguzi wa Naibu Meya

Tarehe iliyowekwa: October 4th, 2023

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam leo tarehe 04 Oktoba, 2023 limefanya Kikao Maalumu katika Ukumbi wa Arnatouglou cha kumchagua Naibu Meya wa Jiji la DSM ikiwa ni kutekeleza kanuni za uchaguzi wa Naibu Meya ambao hufanyika kila baada ya mwaka mmojaambapo katika uchaguzi huo Mhe. Ojambi Masaburi ambaye ni Diwani wa Kata ya Chanika amepita tena kwa kishindo baada ya kupata kura 45 sawa asilimia 100 ya kura zilizopigwa.

Akiongea baada ya ushindi huo, Mhe. Masaburi alitoa shukrani za dhati kwa Chama cha Mapinduzi (CCM) na Waheshimiwa Madiwani wote kwa kuendelea kumuamini na kumpigia kura hivyo kuahidi kushirikiana nao katika kuwatumikia wananchi wa Jiji la Dar es Salaam kwa lengo la kuwaletea maendeleo.

Akitoa salamu zake kwa Baraza la Madiwani baada ya Uchaguzi huo Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Mpogolo amempongeza Naibu Meya kwa kuchaguliwa tena kwani hii inaonesha wajumbe wameamini kazi alizozifanya na kuziomba Kamati ya Fedha pamoja na Kamati ya Uchumi na Huduma za Jamii kuhakikisha wanasimamia miradi ya Maendeleo kwa ukaribu zaidi huku akiwataka kufanya ziara katika shule za Sekondari Ari pamoja na Bangulo lengo likiwa ni kuzifanyia tathmini shule hizo hii ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu yao katika kuhakikisha Wananchi wanapata huduma bora kwa wakati.

Naye Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam Ndg. Jomaary Satura amewataka wajumbe wa Baraza kuhakikisha wanasimamia miradi ya Maendeleo vizuri lengo likiwa ni kuhakikisha Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam inabaki katika uimara wake kwenye ukusanyaji wa mapato na usimamizi mzuri wa Miradi ya Maendeleo.

Aidha kikao hicho kiliambatana na uundaji wa Kamati za Kudumu za Halmashauri pamoja na uchaguzi wa Wenyeviti wa Kamati hizo ambapo Mhe. Saady Khimji akichaguliwa kuwaMwenyekiti wa Kamati ya Uchumi na Huduma za Jamii huku Kamati ya Mipango Miji na Mazingira Mwenyekiti akiwa Mhe. Nyansika Getama na Mhe. Saada Mandwanga akiwa Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili.

Akifunga kikao hicho Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mhe. Omary Kumbilamoto aliwaasa Waheshimiwa Madiwani na Watendaji wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kuvumiliana na kufanya kazi kwa pamoja ili kuweza kuwaletea maendeleo wananchi wa Jiji la Dar es Salaam na Taifa kwa ujumla.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.