• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Mheshimiwa Zungu Akabidhi Madawati 300 Katika Shule ya Sekondari Ilala Kasulu

Tarehe iliyowekwa: March 25th, 2023

Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mussa Azzan Zungu leo tarehe 25 Machi, 2023 amekabidhi madawati 300 katika Shule ya Sekondari Ilala Kasuluiliyopo Kata ya Ilala ambapo Madawati 200 yametolewa na Mheshimiwa Zungu huku madawati 100 yakitoka Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kuhakikisha Ilani ya Chama Cha Mapinduzi inatekelezwa kwa kiasi kikubwa na kuhakikisha Sekta ya elimu inakua katika ufanisi na wanafunzi wote wanasoma katika mazingira bora na tulivu.

Akiongea katika hafla hiyo Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Ilala Mhe. Mussa Azzan Zungu ametoa shukurani zake za pekee kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam pamoja na watendaji wake wote kwa kutatua kero ya madawati katika Shule ya Sekondari Ilala Kasulu huku akiwaahidi kuendelea kushirikiana nao katika kujenga na kuimarisha sekta ya elimu nchini, “Katika kutekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi tumeweza kutoa madawati 300 katika Shule yetu ya Sekondari Ilala Kasulu ambapo Juhudi zote hizi ni kutokana na jitihada za Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa kipaumbele katika Sekta ya elimu kwani kutokana na mchango wake katika kuipa kipambele elimu kwa kujenga Madarasa Katika Shule zetu hivyo na sisi hatunabudi kuleta madawati ili wanafunzi wetu waweze kusoma katika mazingira mazuri na salama.”

Aidha kwa upande wake Mwakilishi wa Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Bi.Tabu Shaibu ameeleza kuwa “Katika utekelezaji wa Ilani ya Chama cha mapinduzi tumeweza kutekeleza na kukuza sekta ya elimu kukua katika ufanisi unaotarajiwa hivyo ni wahakikishie changamoto hizi zitaisha kabisa kwani tutashirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha tunamaliza changamoto zote zinazokabili sekta ya elimu katika Halmashauri yetu.”

Nae Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Ilala Kasulu Mwl. Hamis Ernesti Masatu amesema “Tunamshukuru sana Mbunge wetu pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa kutupatia madawati 300 ambapo kwa kiwango chake tumepunguza idadi ya uhitaji wa madawati katika shule hii ya Sekondari Ilala Kasulu kwani tumepata nyongeza ya madawati takribani 86 hivyo wanafunzi wetu wataweza kusoma katika mazingira tulivu na idadi ya ufaulu itazidi kuongezeka. Pia tunaishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndani ya miaka hii miwili ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu tuliweza kupata fedha za madarasa ya Uviko ila kutokana na ufinyu wa eneo fedha hizo zikahamishiwa sehemu nyingine”.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.