• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam ampongeza Rais Samia kwa kufungua milango zaidi ya uhusiano na miji ya nchi za nje

Tarehe iliyowekwa: June 20th, 2022

Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Jumanne Shauri, amemshukuru na kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimwa Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kufungua milango zaidi inayowaruhusu watu mbalimbali kutoka Miji rafiki ya nje ya nchi kutembelea Tanzania. Shauri ameyasema hayo alipokuwa akiongea na waandishi wa Habari katika mkutano aliouitisha leo tarehe 20 Juni, 2022 kuwajulisha waandishi wa habari kuhusu ujio wa wageni zaidi ya 30 kutoka katika Jiji la Hamburg nchini Ujerumani watakaofanya ziara katika Jiji la Dar es Salaam tarehe 30 Juni, 2022 hadi tarehe 03 Julai, 2022.

Akiongea na waandishi hao wa Habari katika ukumbi wa mikutano wa Old Boma Jijini Dar es Salaam, Shauri amesema kwamba lengo ujio wa ujumbe huo ni kufanya maadhimisho ya miaka 12 ya uhusiano wa Miji Dada kati ya Jiji la Hamburg na Jiji la Dar es Salaam.

“Katika maadhimisho hayo, pande zote mbili zitasheherekea mafanikio yaliyofikiwa hadi sasa katika utekelezaji  wa miradi ya mabadiliko ya tabia ya nchi, afya, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji , michezo na utamaduni, elimu, utalii, stadi za kazi za wanawake, vijana na watu wenye mahitaji maalumu” amesema Shauri.

Katika uhusiano huo Mkurugenzi huyo amesema kumekuwa na fursa nyingi kwa Jiji la Dar es Salaam kufanya ziara za kujifunza na kubadilishana uzoefu wa utendaji kazi katika Jiji la Hamburg na wenzao wa Hamburg pia kufanya ziara kama hizo katika Jiji la Dar es Salaam. Ziara hizo zimewashirikisha pia wadau kutoka asasi za kiraia na mashirika yasiyokuwa ya Serikali.

Aidha, maadhimisho ya Uhusiano wa Miji Dada kati ya Jiji la Dar es Salaam na Jiji la Hamburg, ulioanzishwa tarehe 01 Julai, 2010 baada ya Mamlaka za Majiji hayo kuridhia kuanzishwa kwa uhusiano huo, yanatarajiwa kufanyika tarehe 30 Juni, 2022 hadi tarehe 03 Julai, 2022 ambapo viongozi wa wa majiji hayo mawili watasaini makubaliano ya ya kudumisha uhusiano huo kwa kutoa nafasi kwa wadau wengine zaidi kunufaika na fursa zinazojitokeza kupitia uhusiano huo.

Akihitimisha mkutano huo, Shauri amesema “Sherehe za maadhimisho ya uhusiano huo zitafanyika siku ya Jumapili, tarehe 03 Julai, 2022 katika viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam, hivyo wananchi wote wanakaribishwa kushiriki na kutumia fursa hiyo kwa manufaa ya Jiji la Dar es Salaam.”

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.