• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

RC Makonda aweka jiwe la Msingi la Mradi wa Viwanda Vidogo Vidogo vya Wajasiriamali

Tarehe iliyowekwa: September 9th, 2017

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mheshimiwa Paul C. Makonda leo tarehe 09 Septemba, 2017 ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa viwanda vidogo vidogo vinavyojengwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam katika eneo la Mwananyamala jijini Dar es Salaam ili kuwawezesha wajasiriamali kuboresha ustawi wa maisha yao.

Akiongea katika hafla hiyo Mhe. Makonda ametoa pongezi kwa Waheshimiwa Madiwani na watendaji wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa kujenga na kuboresha mazingira rafiki kwa lengo la kuchochea maendeleo kwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam.

Ameongeza kuwa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi imetaja utaratibu wa kuweka asilimia 10 ya fedha za mapato ya ndani ya Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa ajili ya Wanawake, Vijana na Walemavu na kuagiza kwamba Manispaa za Jiji la Dar es Salaam ziige mfano wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam iliyoanza ujenzi wa miundombinu rafiki kwa wanufaika wa mikopo kwa kuhakikisha kwamba inawajengea miundombinu wanufaika wa mikopo ya Halmashauri katika kila Manispaa za Jiji la Dar es Salaam.

Mhe Makonda amesema mfumo wa sasa hauna utambuzi wa kutosha kwa vijana, wanawake na walemavu kutokana na makundi hayo kutawanyika kibiashara jambo linalosababisha changamoto ya ufuatiliaji wa mikopo hiyo, na kuziagiza Manispaa za Jiji la Dar es Salaam kutenga maeneo maalum ya uanzishaji wa VIWANDA VIDOGO VIDOGO kwa ajili ya makundi hayo, hatua itakayowaweka pamoja na hivyo kutoa fursa kwa Serikali ya Mkoa kuwahudumia vizuri hususan katika kuwawezesha kupata mafunzo ya kuwaongezea ujuzi na utaalamu, masoko na pia kuwaunganisha na Wafanyabiashara wakubwa.

Awali akiwasilisha taarifa kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Bi. Sipora Liana alimweleza Mhe. Paul Makonda kuwa ujenzi wa viwanda hivyo ni sehemu ya utekelezaji wa Kauli Mbiu ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Magufuli, inayochochea uanzishwaji wa viwanda nchini kufikia malengo ya uchumi wa kati ambapo Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, pamoja na kuwawezesha wawekezaji wakubwa wa viwanda kufikia malengo yao na kuwajengea mazingira bora ya uwekezaji, imepanga kujenga viwanda vidogo vidogo kwa ajili ya akina mama, vijana na walemavu wa Jiji la Dar es Salaam pamoja na kuwapatia fedha za mikopo zinayotokana na asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri.

"Katika Mwaka wa Fedha 2016/2017, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ilitenga kiasi cha shilingi 200,000,000.00 kwa ajili ya ujenzi wa viwanda vidogo vidogo ambao utekelezaji wake  ulianza tarehe 01 Juni, 2017 ambapo hadi kufikia mwezi Agosti, 2017 ujenzi wa miundombinu hiyo umefikia asilimia 95. Gharama za mradi huo ni shilingi 199,988,052.00. Ujenzi huo utaendelea kutekelezwa na Halmashauri ya Jiji katika Manispaa za Ilala, Kigamboni, Temeke na Ubungo kwa kadri maeneo yatakavyopatikana", alieleza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji.

Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ambayo inashirikiana na Shirika la Kukuza Viwanda Vidogo Vidogo(SIDO) kuwajengea uwezo wajasiriamali hao itawawezesha kupata mafunzo yatakayowasaidia kuboresha zaidi uzalishaji na biashara zao. Kwa upande mwingine itakuwa rahisi zaidi kwao kupata mikopo kutoka kwenye taasisi za fedha, wadau mbalimbali pamoja na huduma muhimu kutoka Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Mamlaka ya Chakula na Dawa Nchini (TFDA) na wadau wengine.

Kwa kutumia vyombo mbalimbali vya habari vya ndani na nje ya nchi, tovuti ya Halmashauri pamoja na mitandao ya kijami, Halmashauri ya Jiji itawasaidia wajasiriamali hao kujitangaza zaidi ili waweze kupata masoko ya bidhaa zao ndani na nje ya nchi na inatoa wito kwa wajasiriamali wote watakaopata nafasi katika viwanda hivyo kuitunza miundombinu katika maeneo yote yatakayojengwa viwanda hivyo kwa maslahi ya wananchi wote.

Bonyeza hapa kuangalia picha zaidi za tukio hilo.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.