• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Uzinduzi wa mafunzo ya mfumo mpya wa Mipango na Bajeti wa Mamlaka za Serikali za Mitaa

Tarehe iliyowekwa: July 24th, 2017

Mafunzo ya mfumo mpya wa Mipango na Bajeti (Planrep) yamezinduliwa leo Mkoani Mtwara kwa Waganga Wakuu, Makatibu wa Afya, Maafisa TEHAMA, Maafisa  Mipango, Wahasibu,  na Wachumi kutoka katika Mikoa ya Lindi, Mtwara, Ruvuma na Dar es Salaam.

Akifungua mafunzo hayo Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara Bw. Elias Nyabusami amesema mafunzo hayo yamekuja wakati muafaka na yatasaidia kuondoa changamoto mbalimbali zilizokuwa zikijitokeza katika mfumo wa zamani zikiwemo uwepo wa matoleo tofauti tofauti ya mfumo wa mipango na bajeti gharama kubwa zilizotumika pamoja na muda mrefu uliokuwa unatumika wakati wa kuandaa bajeti.

Akifafanua amesema kuwa mfumo huo mpya toleo la mtandao “Web based” utasaidia kutoa mrejesho wa mara kwa mara kwa ngazi husika za utawala kwa wakati na hakutakuwa tena na haja ya wahusika kusafiri  kutoka katika vituo vyao vya kazi ili kushughulikia masuala ya Bajeti na Mipango kwa kuwa sasa yatafanyika katika Mikoa na Halmashauri husika na taarifa hizo kupatikana katika ngazi mbalimbali kwa njia ya mtandao wa intaneti.

Kwa upande wake Mkuu wa timu ya Rasilimali Fedha Kutoka mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma ujulikanao kwa Kiingereza kama “Public Sector Systems Streghthen (PS3)”  Bw. Germini Mtei amesema kuwa kupitia mfumo mpya wa PlanRep Mipango yote na Bajeti za Vituo vya kutolea Huduma kwa wananchi itaonekana kupitia mfumo huo hali itakayosaidia kuongeza ufanisi, uwazi, uwajibikaji na kuboreshwa kwa utoaji huduma.

“Kwa kutumia mfumo huu mpya sasa tunaamini kuwa utasaidia kuondoa ucheleweshaji wa fedha kwenda kwenye miradi na upotevu wa fedha kwa kuwa kila kitu kitafanyika kwa njia ya mtandao” Alisisitiza Bw.Mtei.

Aliongeza kuwa mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya sekta za Umma (PS3) unafadhiliwa na Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani “USAID” ni wa miaka mitano, na utafanya kazi na Serikali Kuu pamoja na Halmashauri 93 katika mikoa 13 ya Tanzania bara katika maeneo yafuatayo:-

  1. Utawala bora na ushirikishwaji wa raia
  2. Raslimali watu
  3. Raslimali fedha
  4. Mifumo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
  5. Tafiti tendaji

Aidha Afisa TEHAMA Mwandamizi toka Ofisi ya Rais TAMISEMI Bw. Archibold Kundasai amesema kuwa mipango yote kuanzia ngazi ya Kata, Halmashauri na Mikoa itakuwa katika mfumo huo na dhamira ya Serikali ni kuongeza tija katika kuwahudumia Wananchi kwa kuhakikisha kwamba mifumo yote ya TEHAMA inazungumza ili kubadilishana taarifa.

“Bajeti ilikuwa ikichukua muda mrefu kuandaliwa ambapo takribani miezi 4 ilitumika ambapo kwa mfumo huu tija itaongezeka kwa kuwa wahusika watabaki katika vituo vyao wakihudumia wananchi huku wakitekeleza jukumu la kuandaa Bajeti na Mipango yao” Alisisitiza Kundasai.

Serikali ya Tanzania na USAID kupitia mradi wa uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3) imeandaa mafunzo haya kwa watumiaji wake nchi nzima. Mafunzo yanatolewa na Wakufunzi kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI, Wakala ya Serikali mtandao, Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Afya na unatarajiwa kutumiwa na watumiaji 1,500 watakaofundishwa matumizi ya mfumo huo.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.