• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Watumishi Idara ya Elimu Msingi Jiji la DSM wamuaga aliyekuwa Afisa Elimu Mama Thomas

Tarehe iliyowekwa: May 22nd, 2021

Na: Hashim Jumbe

Watumishi wa Idara ya Elimu Msingi, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, chini ya Umoja wa Viongozi wa Elimu Jiji la Dar es Salaam (UVEMI) jana tarehe 21 Mei, 2021 wamefanya hafla fupi ya kumuaga aliyekuwa Afisa Elimu Msingi wa Halmashauri hiyo ambayo zamani ilikuwa ikiitwa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala

Hafla hiyo iliyofanyika kwenye ukumbi wa Masia uliopo Segerea, ilihudhuriwa na watu mbalimbali akiwemo Afisa Elimu Mkoa wa Dar es Salaam, Ndugu Abdul Maulid ambaye alikuwa Mgeni rasmi, Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Mhe. Omary Kumbilamoto, baadhi ya Wakuu wa Idara za Halmashauri waliojumuika kwenye hafla hiyo wakiongozwa na Afisa Utumishi Mkuu, Bi. Benadetha Mwaikambo, Wathibiti Ubora wa Shule, Katibu Msaidizi TSC Wilaya ya Ilala, Walimu Wakuu kutoka Shule za Serikali na Shule Binafsi, Maafisa Elimu Kata pamoja na Maafisa wa Idara ya Elimu Msingi waliopo Ofisi ya Idara ya Elimu Msingi Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam wakiongozwa na Bi. Sipora Tenga ambaye ni Afisa Elimu Msingi.

Bi. Elizabeth Thomas amestaafu kwa mujibu wa Sheria ya Utumishi wa Umma akiwa ameihudumia Halmashauri ya Manispaa ya Ilala kwa mafanikio makubwa tangu alipopata cheo cha Afisa Elimu Msingi kuanzia Mei, 2012 hadi Disemba 2020 alipostaafu.

"Mama Thomas alikuwa zaidi ya cheo chake alijipambanua kama Kiongozi, Mlezi, Mshauri na alikuwa Mama wa wote, hakutubagua, wote alituona tupo sawa na kututhamini katika usawa, alitufundisha kazi, na alitamani kuona kila Mtu anafanya kazi kwa moyo na furaha" Mwl. Simon Mndendemi wakati akisoma risala kwa mgeni rasmi

Akizungumza katika hafla hiyo, Afisa Elimu Mkoa wa Dar es Salaam, Ndugu Abdul Maulid, ambaye alikuwa Mgeni rasmi aliwaasa Watumishi waliopo kuendelea kufanya kazi kwa kujituma na kumpa ushirikiano Afisa Elimu mpya "Watumishi mliopo hapa, nyie ni kiungo muhimu katika kumsaidia Mkuu wenu mpya wa Idara kutekeleza majukumu yake, ni matumaini yangu kuwa mtampa ushirikiano wa kutosha kama mlivyokuwa mkimpa Mama Thomas"

Naye Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Mhe. Omary Kumbilamoto alimpa sifa Mama Thomas kwa utendaji wake wa kazi aliokuwa nao "Siku zote nimekuwa nikimsifu Mama Thomas kwa jinsi alivyokuwa akikimbizana kutekeleza miradi yote ya idara yake kama ujenzi wa vyumba vya Madarasa, Ofisi za Walimu, matundu ya vyoo na mengineyo, utendaji wake na kujituma iliturahisishia hata sisi Madiwani, na ilifikia hatua alikuwa akileta taarifa kwenye vikao tunasema tu ipite"

Naye Bi. Sipora Tenga, ambaye ni Afisa Elimu Msingi Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam akimuelezea alivyomfaham Bi. Elizabeth Thomas alisema "Bi. Elizabeth Thomas alikuwa ni mshauri mzuri, alikuwa zaidi ya Mama, na alipenda Watumishi wajiendeleze kielimu na ndiye aliyenifanya niende masomoni kujiendeleza kielimu, wakati huo nikiwa Mwalimu nafundisha Shule ya Msingi Olympio"

Aidha, Mama Thomas amestaafu huku akiacha sifa na heshima kwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ambayo ilikuwa Manispaa ya Ilala, utendaji wake umeifanya Halmashauri hii kufanya vizuri kwenye Taaluma na Michezo, kwani ameisadia Halmashauri kuingia kwenye '10 bora' matokeo ya Kitaifa ya Darasa la Saba na Upimaji wa Darasa la Nne, hakika Jiji la Dar es Salaam wataendelea kumkumbuka kwa mchango wake.

Katika Hafla hiyo Walimu Wakuu wa Shule za Serikali walimpatia mstaafu huyo zawadi ya Gari aina ya 'X-Trail New Model' kama kumbukumbu ya utumishi wake kwa watu aliofanya nao kazi

Tunakupongeza Mama Elizabeth Thomas kwa kuweza kutumikia vyema Halmashauri yetu kwa uadilifu na uaminifu, kwa heri Mama Thomas

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.