• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Waziri Mhagama awataka TARURA kuimarisha Kivuko cha Mwanagati-Magole

Tarehe iliyowekwa: November 22nd, 2023

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Jenista Mhagama (Mb), amewataka Wakala wa Barabara za Vijijini na Mjini (TARURA) kuimarisha kivuko cha Mwanagati-Magole mara tu baada ya mvua kupungua.

Waziri Mhagama ameyasema hayo leo Novemba 22, 2023 alipokuwa akiongea na wananchi wa Mtaa wa Mwanagati na Magole katika ziara yake ya kufanya tathmini na ufuatiliaji wa maeneo yaliyoathiriwa na mvua kwa Mkoa wa Dar es Salaam ambapo eneo mojawapo likiwa ni eneo la daraja linalounganisha Mitaa hiyo ya Kata ya Mzinga Jijini Dar es Salaam.

“Agizo la Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha miundombinu yote yahuduma kutoa huduma kwa wananchi wa Tanzania na ndio maana kutokana na umakini wa Serikali yetu leo tumefika mahali hapa kujionea wenyewe adha wanayoipata wananchi wa Kata ya Mzinga hivyo tumetoa shilingi milioni 20 kwa ajili ya TARURA kuimarisha kivuko hiki hivyo niwaombe wataalamu kutoka TARURA mara tu baada ya mvua kupungua kivuko hiki kiimarishwe ili wananchi waweze kupita muda wote huku mipango ya kujenga kivuko cha muda mrefu ikiendelea kufanyika kwani mvua zikiisha kivuko cha muda mrefu kitaaza utekelezaji, pia nitoe angalizo fedha hizi zitumike ipasavyo isitokee mtu yoyote kuweka mfukoni mwake kwani hatua za kisheria zitachukuliwa na pindi tu mtakapoanza ujenzi  wananchi washirikishwe kwa ukaribu zaidi katika hili,” Amesema Mhe. Mhagama.

Akiendelea kuongea na wananchi wa Kata ya Mzinga Mhe. Mhagama ametoa wito kwa wananchi kuchukua tahadhari kipindi hichi cha mvua hasa wale wanaoishi karibu na mikondo ya maji huku akiwasisitiza kutunza mazingira kwa kuyaweka katika hali ya usafi ili kuepukana na magonjwa ya mlipuko kama Kipindupindu ambayo hutokea kipindi hiki cha mvua.

Kwa Upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila ameema “Tunaishukuru Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kuja kuona hali halisi ya namna ilivyo lakini nipende kuwaambia mpaka sasa Dar es Salaam hakuna mafuriko bali kwa wananchi wa Mzinga adha yao kubwa ni miundombinu ya Daraja pamoja na miundombinu ya barabara ambayo imeharibiwa na mvua hivyo niwahakikishie adha hii inakwenda kuisha kwani tayari TARURA wameshachora mchoro wa kujenga daraja hili ambao utagharimu shilingi bilioni 1.7 lakini pia kwa upande wa barabara DMDP awamu ya pili barabara hii imeingia kwenye mradi huu hivyo itatengenezwa barabara ya kiwango cha lami yenye KM 7 itakayoka kwa Mpalange Mpaka kuunganisha barabara ya Mwanagati inayopitia Banana hivyo niwaombe mume wavumilivu kwani kero zenu tumezisikia na tunazifanyia kazi.”

Awali akiongea wakati wa ziara hiyo Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Mpogolo Ametoa shukrani zake kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi nzuri anayoifanya ya kuhakikisha Wananchi wanapata huduma kwa wakati huku akimuhakikishia Waziri Mhagama kusimamia kwa ukaribu zaidi yote atakayoyaelekeza.


Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.