• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

DC Ilala awataka Madiwani na Viongozi wa Halmashauri ya Jiji la DSM kusimamia Miradi ya Maendeleo ikamilike kwa wakati

Tarehe iliyowekwa: October 19th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Mpogolo amewataka Waheshimiwa Madiwani kwa kushirikiana na viongozi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kuhakikisha wanasimamia vyema utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo kwa ukaribu zaidi ili ikamilike kwa wakati, hayo ameyasema leo Oktoba 19, 2023 Katika Ukumbi wa Arnatouglou Jijini Dar es Salaam wakati wa kikao maalumu cha Madiwani kupitisha taarifa ya ujenzi wa masoko ya kisasa.

Akizungumza katika kikao hicho Mhe. Mpogolo amesema “Lengo la kikao hichi ni kuwaasilisha michoro ya majengo ya Masoko ya kisasa yanayoenda kutekelezwa katika Halmashauri yetu ikiwemo Soko la Ilala na Mchikichini ambayo yatakwenda kutuongezea mapato zaidi yatakayo tumika kuendeleza sekta nyingine za Afya pamoja na Elimu ikiwa ni kutekeleza adhima ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuboresha miundombinu na kuwapanga wafanyabiashara kufanya biashara katika maeneo maalumu hivyo niwaombe Waheshimiwa Madiwani kwa kushirikiana na viongozi wa Jiji la DSM msimamie miradi hii iweze kukamilika kwa wakati kwani jitihada za kuongeza mapato ndio zimeleta miradi hii ya kimkakati kwakua ujenzi wa Masoko haya utatusaidia kuwatambua wafanyabiashara na kudhibiti upotevu wa mapato.”

Sambamba na hilo Mhe. Mpogolo amewataka viongozi hao kushirikiana na kuwataka Waheshimiwa Madiwani kuainisha maeneo ya wazi yanayopatikana kwenye Kata zao kwani kupitia maeneo hayo miradi mingi itaendelea kutekelezwa kwa Kasi zaidi.

Kwa Upande wake Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Mhe. Omary Kumbilamoto amemuhakikishia Mkuu wa Wilaya ya Ilala kutekeleza yote aliyoelekeza huku akimuahidi kuwa atashirikiana na Kamati zake za kudumu za Halmashauri kusimamia miradi hiyo ipasavyo ili ikamilike kwa wakati ikiwa ni sehemu ya kuboresha miundombinu pamoja na utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salam Bw. Jomaary Satura ameeleza kuwa lengo la kikao hicho ni kuwashirikisha Madiwani katika utekelezaji wa miradi hiyo ya kimkakati ili waweze kutoa maoni kwani anaamini kupitia miradi hiyo Halmashauri itaenda kukusanya mapato kwa wingi na kupita lengo hata hivyo baada ya kuanzishwa Kanda saba za Huduma Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam robo ya Kwanza (Julai hadi Septemba) imeweza kukusanya kiasi cha shilingi bilion 31.5 hii inaonesha ni jinsi gani Jiji la Dar es Salaam limejikita katika kukusanya mapato na kuhakikisha huduma zinawafikia wananchi kwa ukaribu zaidi.

Aidha, katika kikao hicho wajumbe waliweza kufundishwa jinsi ya kuboresha na kupendezesha Mandhari ya Jiji la Dar es Salaam, namna ya kuitangaza Halmashauri katika utalii wa ndani, kuboresha eneo la Mnazi Mmoja kuwa la maegesho ya magari pamoja na kutenga eneo kwa ajili ya bandari kavu kwani kupitia miradi hii mapato ya Halmashauri yatazidi kuongezeka kwa kiwango kikubwa.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.