• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Kamati ya Uchumi na Huduma za Jamii Jiji la DSM yafanya Ziara ya ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo

Tarehe iliyowekwa: February 13th, 2023

Kamati ya Uchumi na Huduma za Jamii ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, imefanya ziara ya kawaida ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa Fedha 2022/2023 (Oktoba hadi Desemba2022) Ambapo walitembelea Shule za Sekondari Viwege na Mvuti na Shule ya Msingi Kigogo Fresh.

Akizungumza kwenye ziara hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi na Huduma zaJamii Mhe. Robert Manangwa ameeleza kuwa wameridhishwa na Ubora wa shule na kumpongeza Kaimu Mkurugenzi pamoja na Watumishi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa usimamizi wa fedha za Serikali.

Naye, Mkuu wa Shule ya Sekondari Viwege iliyopo Kata ya Majohe Bi. Kalunde Sigera ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kuendelea kuboresha miundombinu katika shule hiyo ambapo amebainisha kuwa katika shule yake kuna miradi minne ambayo tayari imetekelezwa kwa mwaka 2022/2023 ambayo ni ujenzi wa vyumba sita vya madarasa, ujenzi wa bwenj la Wasichana, jengo la Utawala pamoja na Maabara mbili ya Baiolojia na Kemia.

"Shule ilipokea Shilingi Milioni 120 kutoka Serikali Kuu maarufu kama ‘Pochi ya Mama’ kwa ajili ya ujenzi wa vyumba sita vya madarasa, kiasi cha Sh. Milioni 118.9 zimetumika kujenga vyumba sita vya madarasa, Ofisi mbili za walimu, Madawati, Viti na Mezatumepata 30 pia tumelipia service line ya TANESCO ili jengo hili liwe na umeme wake peke yake ambao utaunganishwa pia kwenye Jengo tunalolijenga la maabara" Amesema Bi. Karunde.

Vilevile Bi.Kalunde ameongeza kwa kubainisha fedha walizopata kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ambayo ni sh. Milioni 120 kwa ajili ya ujenzi wa Bweni la Wasichana na fedha iliyotumika ni sh.Milioni 51.5 ujenzi unatarajiwa kukamilika ifikapo tarehe 28 Machi 2023, Ujenzi wa Jengo la Utawala umepokea sh. Milioni 65 kutoka mapato ya ndani na mpaka sasa imetumika sh. Milioni 31.7 ambao ujenzi huo nao unatarajiwa kukamilika ifikapo tarehe 28 machi 2023 sambamba na sh. Milioni14 zilizotolewa kwa ajili ya ujenzi wa Maabara baada ya Maabara iliyokuwepo kuungua.

Kwa upande wake Mwl. Gasper Mwaipopo Mkuu wa Shule ya Sekondari Mvuti naye amemshukuru Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuwaletea mradi huo ambao umetoa fursa kwa wanafunzi kupata elimu iliyo bora pamoja na viongozi wengine ambao wameshiriki vyema na kubainisha miradi miwili ambayo wameitekeleza katika shule yake 2022/2023 ambao ni mradi wa Bweni unaoendelea pamoja na Mradi wa Pochi ya Mama ambao umejikita katika ujenzi wa madarasa tisa ulioanza tarehe 3 Novemba na kuthibitisha mpaka sasa Mradi huo tayari umekamilika kwa asilimia 100

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.