• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Soko la Kariakoo kuwa la Kimataifa

Tarehe iliyowekwa: March 27th, 2024

SERIKALI imeendelea kuwahakikishia wafanyabiashara wa Soko la Kariakoo kuwa la Kimataifa zaidi, kutokana na uboreshwaji inaoenda kufanyika katika soko hilo, kwa kuweka Miundombinu rafiki kwa watu wote wanaofika katika soko hilo kutoka pembe zote za Afrika Mashariki, kupata huduma masaa 24 na uimarishaaji wa ulinzi.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Machi 27, 2024 Ofisini kwake Jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mhe. Edward Mpogolo, amesema wamekuwa na vikao mbalimbali na viongozi wa Wafanyabiashara pamoja na Machinga, lengo likiwa ni kufahamu changamoto mbalimbali zinazowakumba Wafanyabiashara hao katika soko la Kariakoo.

“Wote tunajua ukubwa wa soko hili na mahitaji mbalimbali ambayo watu wamekuwa wakijipatia na kufanya idadi kubwa ya wateja kufika sokoni hapo, hivyo lazima na serikali kwa kushirikiana na Mwenyekiti wa Wafanyabiashara na Mwenyekiti wa Wamachinga kuhakikisha wanabainisha changamoto zao ili ziweze kupatiwa ufumbuzi wa haraka kabla ya kukarabatiwa kwa soko hilo.” amesema Mhem Mpogolo.

Aidha amesema, kikao hicho kimekuwa na makusanyo ya changamoto, ikiwemo wafanyabiashara kuegesha biashara zao nje ya maduka na kurasimisha kama eneo sahihi la kuendesha biashara hizo na kuleta ugumu kwa kupatikana njia katika soko hilo.

“Unakuta Muuza magodoro ameweka bidhaa hizo dukani na pia ametoa hadi nje ya duka lake na kusababisha mrundikano wa bidhaa hizo hadi sehemu ya barabarani ,alikadhalika wauzaji wa Mafriji ni hivyo hivyo na inasababisha changamoto ya kulipa kodi sahihi na kupunguza thamani ya soko la Kariakoo” ameongeza.

Hata hivyo, Mhe. Mpogolo ameeleza kuwa, Serikali imeadhimia kuanza mara moja ukarabati wa soko hilo kwa kuanza kuweka taa na tayari baadhi ya mitaa imeshaanza kuweka taa hizo ikiwemo Mtaa wa Mkunguni na mchikichini na taa hizo zitawekwa mtaa wa Tandamti na Nyamwezi.

“Kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi tunatekeleza hatua hizo za ukarabati wa awali wa kuweka taa hizo ili kuwepo kwa usalama zaidi kwa wateja ambao wanafika muda ambao wa jioni zaidi ama usiku hivyo itawarahisishia kuwepo kwa mwanga ambao kimsingi itawajengea amani na usalama eneo hilo kwa mteja au mfanyabiashara mwenyewe.” ameongeza.

Pia amesema, katika kikao hicho wamefikia muafaka wa kuhakikisha wafanyabiashara wa kushusha mizigo (Kirikuu) kupatiwa eneo stahiki la kushusha mizigo yao ili kuepusha misongamano pamoja na wafanyabiashara wanaoweka bidhaa zao chini watatakiwa kurudi kwenye maeneo yao rasmi waliyokwisha pangiwa.

Hata hivyo Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Jomaary satura, ameongeza kuwa jambo hilo la mkakati wa ukarabati wa soko hilo limekuwa shirikishi na limeweza kujadili changamoto mbalimbali kwakina na kwa pamoja tumeona tusipochukua hatua hizi kwa haraka na kwa ufanisi hatutaweza kufikia malengo ya soko la Kimataifa.

Pia amesema ukarabati huo utawawezesha wafanyabiashara hasa kipindi hiki cha kuelekea sikukuu kupata mahitaji masaa 24 kwa usalama zaidi kutokana na kuwepo kwa taa na kamera.

Kwa Upande wake Makamo Mwenyekiti wa Wafanyabiashara soko la Kariakoo, Steven Lusinde, ametoa pongeza kwa Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ndani ya Miaka mitatu imekuwa ya Maendeleo na mabadiliko katika sekta mbalimbali na kuwaona wafanyabiashara wanahitaji maboresho mbalimbali, ili waweze kufanya biashara zao kwa ufanisi zaidi .

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.