• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

DC Ludigija afungua mashindano ya UMITASHUMTA ngazi ya Wilaya kwa mwaka 2022

Tarehe iliyowekwa: July 1st, 2022

Na: Hashim Jumbe

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mhe. Ng'wilabuzu Ludigija, leo tarehe 01 Julai, 2022 amefungua rasmi mashindano ya umoja wa michezo na taaluma kwa shule za msingi Tanzania, maarufu kama  UMITASHUMTA kwa ngazi ya Wilaya ya Ilala.


Mashindano hayo yanayofanyika kwa siku 3 kwenye viwanja vya Shule ya Kebby vilivyopo Pugu Kinyamwezi, yalianzia kwa kushindanishwa timu za madarasa, shule, kata na hatimaye kufikia kutengeneza timu za Klasta, ambazo leo zimeanza kushindanishwa ili kutengeneza timu itakayowakilisha Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwenye ngazi ya UMITASHUMTA Mkoa.


"Mheshimiwa Mgeni rasmi, mbele yako ni wanamichezo 480 pamoja na walimu wao kutoka Klasta za Chanika, Ukonga, Kimanga na Gerezani ambao leo wanaanza rasmi Mashindano ya UMITASHUMTA ngazi ya wilaya. Mashindano haya yanashirikisha michezo ya wavu, soka, riadha, netboli, mpira wa mikono, ngoma na kwaya" alisema Bi. Asha Mapunda ambaye ni Afisa Elimu Michezo wa Idara ya Elimu Msingi Jiji la Dar es Salaam


Naye Afisa Elimu Msingi Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Bi. Sipora Tenga akiongea wakati akimkaribisha Mgeni rasmi alisema "Wilaya yetu imekuwa ikifanya vyema sana katika mashindano ya UMITASHUMTA na hata taaluma. Mwaka 2021 tuliweza kupata nafasi ya kwanza kitaifa kwa upande wa ngoma na nafasi ya 8 upande wa kwaya, pia tuliweza kutoa idadi kubwa ya wachezaji  72 kati ya 100 ambao ni sawa na 70% kwa  waliounda  timu ya  Mkoa wa Dar es salaam"


Mashindano ya UMITASHUMTA kwa mwaka 2022 yanabeba kauli mbiu isemayo  “TAKWIMU SAHIHI NI MSINGI WA MIPANGO BORA YA TAIFA” SHIRIKI SENSA YA WATU NA MAKAZI KWA MAENDELEO YETU.


Naye Mkuu wa Wilaya ya Ilala wakati akifungua mashindano hayo aliwakumbusha wanafunzi hao lengo la wao kuwepo hapo "lengo la mashindano haya ni kushindanisha wanafunzi katika  michezo mbalimbali ili kuibua vipaji vya vijana watakaounda timu bora ya wilaya na baadaye kushiriki mashindano ya UMITASHUMTA Mkoa wa Dar es salaam, niwaase kucheza kwa juhudi ili tupate timu itakayokwenda kushindana ngazi ya Mkoa na kuibuka washindi, siku zote Ilala sisi ni washindi" Mhe. Ng'wilabuzu Ludigija


Ikumbukwe kuwa timu ya Wilaya ya Ilala ndiyo inayoshikilia ubingwa wa UMITASHUMTA kwa ngazi ya Mkoa wa Dar es Salaam kwa miaka minne (4) mfululizo, hivyo kuwa na nafasi nzuri kwa mwaka huu kushinda kwa mara ya tano (5) mfululizo.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.