Na: Shalua Mpanda
Wakazi wa Mkoa wa Dar es Salaam na Mikoa ya jirani, wametakiwa kujitokeza kwa wingi katika zoezi la uchunguzi na upasuaji wa mabusha ulioanza rasmi Januari 5,2026,katika halmashauri za mkoa huo.
Akizungumza na waandishi wa habari kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila, Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Mhe. Saad Mtambule amesema Serikali imegharamia matibabu hayo hivyo wananchi hawana budi kujitokeza katika maeneo yao.
Ameyataja baadhi ya maeneno ambayo huduma hiyo ya uchunguzi na upasuaji inatolewa hadi Januari 30 ni vituo vya afya Kinondoni wilaya ya kinondoni na Kilakala kilichopo wilayani Temeke.
"Tumieni siku hizi 25 zilizotolewa na Wizara ya Afya kwenda kwenye vituo hivi, wataalamu wapo wa kutosha na siku ni nyingi, wafahamisheni ndugu na jamaa wakapate huduma hii". Alisisitiza Mhe. Mtambule
Kampeni hii kwa mkoa wa Dar es Salaam inalenga kuwafikia watu 500 ambapo mpaka sasa zaidi ya watu 160 wameshafanyiwa uchunguzi na 127 kati yao wamepangiwa tarehe za kufanyiwa upasuaji
1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM
Anuani ya Posta: S.L.P 20950
Simu ya mezani: 0738 378 386
Namba ya Mkononi: 0738 378 386
Barua Pepe: info@dcc.go.tz
Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.