• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

DC Ilala Awataka Wananchi kuweka Jiji Katika Hali ya Usafi

Tarehe iliyowekwa: February 25th, 2023

Katika kuendeleza na kutekeleza kampeni ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe.Amos Makaka Mkuu wa Wilaya ya Ilala Leo Februari 25,2023 ameshiriki zoezi la usafi katika Kata ya Kariakoo ambapo usafi huo ulijumuisha maeneo ya Barabara ya Bibi Titi, Barabara ya Nkurumah pamoja na maeneo ya barabara ya Lumumba na Barabara ya Morogoro.

Zoezi hilo lililoongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Mpogolo akiambatana na Katibu Tawala wa Wilaya ya Ilala, Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Diwani wa Kata ya Gerezani na Jangwani, Watumishi kutoka Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Watendaji wa Mtaa, viongozi wa Chama cha Mapinduzi wa Kariakoo Mashariki, viongozi kutoka shujaa wa maendeleo na Ustawi wa Jamii Tanzania (SMAUJATA), wadau kutoka Bank ya CRDB na wadau mbali mbali wa usafi wakiwemo Wejisa Company limited, Kajenjere Trading Company Limited, Sateki Trading Limited, Umoja wa Madereva wa Pikipiki Mjini Kati, Vingunguti na Msimbazi Jogging Club pamoja na Wananchi wa Kata ya Kariakoo.

Aidha, Mhe.Edward Mpogolo amewashukuru viongozi wa Machinga na Bodaboda kwa kuweza Kuhudumu katika Barabara ya Lumumba hivyo ameelekeza Vigingi na Miti kutoka barabara ya Airport vihamishwe na kuletwa barabara ya Lumumba ili kuboresha eneo hili.

“Kutokana na ukubwa wa Barabara ya Lumumba napenda kuwaomba watu wa maduka waboreshe maeneo yao huku upande wa katikati ya barabara tutahakikisha Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam tunashirikiana na Wamachinga, Bodaboda pamoja na wadau mbalimbali ili kuhakikisha barabara hii inakuaje safi na bora kwani Dar es Salaam hususani Wilaya ya Ilala kwani ndiyo Kitovu cha kupokea wageni wanaoingia Nchini.”

Sambamba na hilo Mhe. Mpogolo amemuelekeza Mkurugenzi wa Jiji kwa kushirikiana na watendaji wake kuhakikisha wanaandaa barua na Kuwapelekea wafanyabiashara wote wenye Majengo kuanzia barabara ya Airport hadi Ikulu ili kuona namna gani watawaelekeza kuboresha mazingira na miti gani waweze kupanda kwenye maeneo yao ili kuboresha mazingira ya Mji wetu.

Aidha Mhe. Mpogolo amewataka vijana wote wanaobandika stika maeneo ya Lumumba kuhakikisha wanaweka Jiji safi baada ya kumaliza kazi zao. Akiendelea kuongea katika zoezi Hilo Mhe.Mpogolo ameelekeza vifusi vyote vya mchanga vilivyopo barabarani kuondolewa pia watu wa ustawi wa jamii watafute namna ya kuwaelekeza watu wote wanaolala kando ya barabara na ndani ya Viwanja wahakikishe wanawaondoa katika maeneo hayo kwa kutumia utaratibu maalumu huku akiwataka wanaoegesha magari maeneo ambayo sio ya maegesho kupigwa faini kwani ni moja ya uchafuzi wa mazingira.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam Eng. Amani Mafuru ameeleza kuwa kampeni hii ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam imekua ya mafanikio zaidi kwa Jiji la Dar es Salaam kuwa Safi kwani wananchi wameonekana kujitokeza kwa wingi katika zoezi la usafi.

“Nipende kutoa Shukrani zangu za dhati kwa Mkuu wa Mkoa Wa Dar es Salaam Mhe.Amos Makalla kwa kuanzisha Kampeni hii ambayo ni endelevu kwani kutoka na kampeni hii Mkoa wa Dar es Salaam umeweza kushika nafasi ya Sita barani Afrika kwa usafi hivyo niwaombe wananchi kuhakikisha usafi ni Sehemu ya maisha yetu ya Kila siku na si mpaka tusubiri usafi wa mwisho wa mwezi.” Ameeleza Eng. Mafuru.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.