• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Jiji la DSM lapitisha Mapendekezo ya Mpango na Bajeti ya Tshs. Bilioni 278 kwa mwaka 2024/25

Tarehe iliyowekwa: February 20th, 2024

BARAZA la Madiwani Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, leo Tarehe 20 Februari, 2024 limefanya Mkutano Maalum wa Mapitio ya Mpango na Bajeti ya Mwaka 2023/2024 kwa kipindi cha nusu mwaka (Julai-Desemba, 2023) na kufanya Makadirio ya Mpango na Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2023/2024 wenye Jumla ya Tshs. Bilioni 278, ambapo kati ya fedha hizo kiasi cha Tshs. Bilioni 130 sawa na 47% ya Bajeti yote ni makusanyo kutoka vyanzo vya mapato ya ndani ya Halmashauri na Shilingi Bilioni 148 sawa na 53% ya Bajeti ni fedha za Ruzuku kutoka Serikali Kuu.

Aidha, kikao hicho kilichofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa Arnatouglou na kuongozwa na Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mhe. Omary Kumbilamoto, kilipokea, kikajadili na kisha kupitisha Rasimu ya Mpango na Bajeti ya mwaka wa fedha 2024/2025 ambapo Bajeti hiyo imekua na ongezeko la jumla ya Tshs. Bilioni 40.9 sawa na 46% kutoka katika mapato ya ndani ikilinganishwa na bajeti ya mwaka 2023/24, hii imetokana na mikakati bora iliyowekwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwenye ukusanyaji wa mapato na uibuaji wa vyanzo vipya vya mapato.

Katika Makadirio ya Mpango na Bajeti ya mwaka 2024/2025 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imeweka vipaumbele vitano (05) vitakavyolenga kutatua changamoto kwa ustawi wa wananchi wa Jiji la Dar es Salaam

Akisoma taarifa kuhusu makadirio ya mpango na bajeti ya mwaka 2024/2025 mbele ya Baraza la Madiwani, kwa niaba ya Mkurugenzi wa Jiji, Bw. Julius Ndele alisema "Kwa mwaka wa fedha 2024/2025 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imepanga kukusanya Shilingi Bilioni 130 kutoka kwenye vyanzo vyake vya ndani."


Matumizi ya Mapato ya ndani ya Halmashauri kwa mwaka 2024/2025

Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa mwaka wa fedha 2024/2025 kwenye mapato yake ya ndani inatarajia kutumia fedha kiasi cha Tshs. Bilioni 130 katika mchanganuo ufuatao; Matumizi ya kawaida Tshs. Bilioni 21.3 sawa na 16.3%% ya Bajeti, Miradi ya Maendeleo Tshs. Bilioni 74.4 sawa na 57.2% ya Bajeti, Mishahara Tshs. Bilioni 2.2 sawa na 1.6% na Vyanzo Fungiwa Tshs. Bilioni 31.9 sawa na 24.5% ya mapato ya ndani.

Ruzuku ya Tshs. Bilioni 148 kutoka Serikali Kuu imegawanywa katika maeneo mawili ambayo ni Matumizi ya Kawaida na Miradi ya Maendeleo


Mchanganuo wa Matumizi ya kawaida kwa fedha ya Ruzuku

Kwa mwaka wa fedha 2024/2025 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam inatarajia kutumia Tshs. Bilioni 122.4 ya fedha ya ruzuku sawa na 82.4% kulipa Mishahara na Tshs. Bilioni 1.2 sawa na 0.85% kwa ajili ya Matumizi Mengineyo


Mchanganuo wa Fedha za Miradi ya Maendeleo kwa fedha ya Ruzuku

Katika kipindi kijacho cha 2024/2025 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imepanga kutumia Tshs. Bilioni 24.3 kutekeleza Miradi ya Maendeleo ambayo ni sawa na 16.4%.

Katika kuandaa Rasimu ya Mpango na Bajeti ya mwaka wa fedha 2024/2025 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imeandaliwa kwa kufuata na kuzingatia Sheria ya Bajeti namba 11 ya mwaka 2015, mwongozo wa maandalizi ya bajeti (PBG) ya mwaka 2024/25, Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020-2025, Mpango mkakati wa Halmashauri (SP), Mpango wa maendeleo wa miaka mitano (5YDP III 2020/2021 – 2025/2026), Malengo ya maendeleo endelevu (SDGs), Waraka wa Hazina namba 4 wa mwaka 2024 pamoja na maelekezo mahsusi ya viongozi mbalimbali wa Serikali katika Halmashauri yetu kwa nyakati tofauti.

















Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.