• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Kamati ya Lishe Halmashauri ya Jiji la DSM yafanya Kikao cha kujadili taarifa za utekelezaji wa kazi za Lishe kwa Kipindi cha Robo ya Nne

Tarehe iliyowekwa: September 19th, 2023

Kamati ya Lishe Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam leo Septemba 19, 2023 wamefanya kikao cha kawaida cha Kujadili taarifa za utekelezaji wa Kazi za Lishe kwa kipindi cha robo ya nne kuanzia Aprili hadi Juni 2023.

Akifungua kikao hicho Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Bi. Tabu Shaibu amesema kuwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam inatekeleza maagizo ya upatikanaji wa lishe kwa vitendo kwani Serikali ya Tanzania imedhamiria kuendelea kulipa umuhimu wa kipekee suala la lishe bora nchini kwani ni suala mtambuka hivyo kamati ya lishe ihakikisha inajikita zaidi kuhamasisha na kutoa elimu kuhusu mlo kamili na namna ya uandaaji wa mlo huo huku akiwakumbusha wajumbe wote wa kamati ya lishe kuhakikisha mambo waliyokubaliana katika kikao hicho yanafanyiwa kazi ili kufikia malengo waliojiwekea.

Katika kikao hicho Divisheni mbali mbali ziliwasiliisha taarifa za utekelezaji wa kazi za lishe kwa kipindi cha robo ya nne ambapo baada ya taarifa hizo Kamati iliweza kujadili na kutoa maelekezo kwa Divisheni ya Elimu Sekondari kuhamasisha zaidi suala la lishe kwa wanafunzi kwani inaonekana Shule nyingi za Sekondari na Msingi wanafunzi hawapati mlo kamili.

Vilevile kwa upande wa Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Afisa Kilimo Bi. Fatuma Mahanaka amesema suala la kutoa elimu kwa wakulima na wafugaji limetekelezwa kwa kutoa ushauri na elimu ikiwa ni pamoja na kuwasisitiza kuhifadhi vyakula na kuweka akiba ya mifugo kwa matumizi ya baadae huku akiahidi kuendelea kushirikiana na Idara za Elimu Sekondari  naMsingi kuendelea kutoa elimu ya lishe shuleni hususani kuwafundisha wanafunzi namna ya kulima kilimo cha uyoga kwani uyoga ni zao zuri kwa kuboresha Afya ya akili na ya mwili pia.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Dkt. Zaituni Hamza ameeleza kuwa “Afua ya Lishe inasimamiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tusimuangushe tusimame nae bega kwa bega kuhakikisha masuala ya elimu na utekelezaji wa afua za lishe kwa wanafunzi na jamii kwa ujumla hivyo niwasihi sana kuimarisha masuala ya lishe kwenye jamii zetu kwani lishe imekua ni changamoto na nitoe wito kwa kila mjumbe aifanye ajenda na kutembea nayo kuelimisha wananchi kuhusu mlo kamili na aina ya vyakula vinavyostahili kuliwa hivyo Divisheni ya Kilimo   mhakikishe mnatoa mchango wenu wa kusimamia namna ya bora ustawishaji wa mazao kwa afya bora.”

Aidha katika kikao hicho wajumbe walikubaliana katika kuongeza jitihada zaidi katika kuandaa programu za kuhamasisha na kutoa elimu za mara kwa mara kwa wananchi juu ya masuala ya lishe hususani mashuleni na kwa mama lishe ili kuboresha Afya za wananchi kwa maendeleo ya Nchi.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.