• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Kamati ya Siasa Wilaya ya Ilala Yaridhishwa na utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

Tarehe iliyowekwa: March 14th, 2023

Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ilala yaridhishwa na matumizi ya fedha na kasi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa kupitia fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam.

Hayo yameelezwa na Mwenyekiti CCM Wilaya ya Ilala Ndg. Said Sidde leo tarehe 14 Machi, 2023 akiwa na Wajumbe wa Kamati ya Siasa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi mbalimlbali ya maendeleo inayotekelezwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa mwaka 2021/2022.

Miradi iliyotembelewa na Kamati hiyo ni pamoja na ujenzi wa Kituo cha Afya Mchikichini kinachotekelezwa kwa fedha za mapato ya ndani takribani shilingi Bilioni 5.2 kikiwa hatua ya Frame Work (Boma) na hadi kufikia Novemba 2023 kituo hicho kitakamiliki,ujenzi wa ukaguzi wa mazingira ya dampo la Pugu Kinyamwezi ambapo Serikali ya Uholanzi kwa kushirikiana na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam wametoa msaada wa Bilioni 2 kwa ajili ya uboreshaji wa udhibiti wa miundombinu ya taka ngumu, Ukaguzi wa Kivuko cha Mgeule kinachotekelezwa kwa kutumia fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri ambapo kivuko hicho kimetekelezwa kwa asilimia 54.32% na hadi kukamilika kivuko hicho kitatumia takribani shilingi milioni 614.8, ukaguzi wa ujenzi wa ghorofa lenye sakafu 5 zenye madarasa 20 na matundu 45 ya vyoo katika Shule ya Sekondari Bonyokwa ambapo ujenzi huo upo hatua ya Jamvi na hadi kufikia Oktoba 2023 ujenzi unatarajiwa kukamilika na utagharimu takribani shilingi bilioni 1.7 zikiwa ni fedha kutoka mapato ya ndani ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Ukaguzi wa barabara ya kiwango cha Lami Kasongo Mtaa wa Mafuriko yenye urefu wa mita 341 milioni ambayo imetekelezwa kwa fedha takribani shilingi milioni 456 zikiwa ni fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri.

Aidha Wajumbe hao pia walipata fursa ya kutembelea Mradi wa Kikundi cha Boda Boda TITANIC ambao ni wanufaika wa Asilimia 10% ya mapato ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ambapo kwa awamu ya kwanza vijana hao walipewa shilingi milioni 12 ambazo zilitumika kununua Pikipiki tano (5) baada ya kurejesha mkopo huo wakapewa tena kiasi cha shilingi Milioni 50 ambazo wamefungua duka la huduma za miamala ya simu huku kikundi hicho kikiweza kurejesha shilingi milioni 13 mpaka sasa, aidha kikundi cha vijana ni muunganiko wa vijana saba (7) ambao walitokea mazingira magumu na wengine walikua waathirika wa madawa ya kulevya.

Akihitimisha ziara hiyo Mwenyekiti wa kamati ya Siasa Wilaya ya Ilala Ndg. Said Sidde amesema “Naipongeza sana Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa utekelezaji wa miradi kwani thamani ya fedha inaonekana pia miradi inatekelezwa kwa kiwango cha juu zaidi hii inaonyesha ni jinsi gani Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) inavyotekelezwa kwa kasi zaidi.”

Sambamba na hilo Bw.Sidde ameeleza kuwa katika dampo la Pugu Kinyamwezi ambalo linaonekana kuwa na wafanyakazi takribani 600 ambao wanaokota taka kwa ajili ya viwanda hivyo ameelekeza kuwa kama ikiwezekana Halmashauri waanzishe sheria ndogo kwa ajili ya kupata mapato kwa yale makampuni yanayochukua taka kwenye dampo kwa ajili ya kuzalisha vitu mbalimbali.

Akiongea kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Katibu Tawala wa Wilaya ya Ilala Bi. Charagwa Selemani amemuhakikishia mwenyekiti wa kamati ya Siasa Wilaya ya Ilala kutekeleza yote aliyoyaagiza lengo likiwa ni Kutekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) pamoja na kusogeza huduma za kijamii karibu na Wananchi.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.