• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Karibu Mwenge Maalum wa Uhuru 2021 Wilaya ya Ilala

Tarehe iliyowekwa: August 13th, 2021

Na: Hashim Jumbe 

TAREHE 08 Desemba, 1961 muda mchache kabla ya kutimia Saa 6:00 Usiku, Luteni Alexander Gwebe Nyirenda alikuwa juu ya kilele cha Mlima Kilimanjaro akiwasha Mwenge, tukio ambalo lilikwenda sambamba na kupandishwa kwa bendera ya Taifa jipya la Tanganyika wakati bendera ya Uingereza ilipokuwa inateremshwa kwenye Uwanja wa Taifa wa Uhuru, Mkoani Dar es Salaam.

"Sisi tumekwisha uwasha Mwenge wa Uhuru na kuuweka juu ya Mlima Kilimanjaro, umulike ndani na nje ya mipaka yetu, ulete matumaini pale ambapo hakuna matumaini, ulete upendo mahali penye chuki na heshima mahali palipo jaa dharau” maneno ya Mwalimu Nyerere wakati akitoa hotuba ya siku ya Uhuru, Tarehe 09 Desemba, 1961 akiwatangazia Watanganyika, Afrika na Dunia kwa ujumla

Aidha, baada ya Uhuru wa Tanganyika na kuwashwa kwa Mwenge wa Uhuru, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na viongozi wenzake walielekeza juhudi zao katika kuwaunganisha Watanzania na kuweka misingi imara ya kulijenga Taifa huru la Tanganyika, kudumisha amani, upendo, umoja, mshikamano na kuweka sera za kukabili maadui ujinga, umaskini na maradhi.

Itakumbukwa kuwa Mwenge wa Uhuru umekuwa ukikimbizwa Nchi nzima ukipita kwenye mitaa na umeendelea kuwakumbusha Watanzania wajibu wa kufanya kazi kwa bidii ili kuleta maendeleo huku ukitumika kuzindua miradi mbalimbali kila mwaka kwenye maeneo unakopita.

Kwa mwaka 2021 Mbio za Mwenge wa Uhuru ni Mbio Maalum na  umaalum wake pia unatokana na Mbio hizi za Mwenge wa Uhuru kukimbizwa kwa Siku 150 katika Wilaya 150 za kiutawala tu za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania badala ya Halmashauri za Wilaya 195 kama ilivyozoeleka

Kwa Wilaya ya Ilala, Mwege huo wa Uhuru utakimbizwa Tarehe 18 Agosti, 2021 na unatarajiwa kuzindua, kukagua na kuweka mawe ya msingi katika miradi mbalimbali ya kimaendeleo iliyotekelezwa, na moja kati ya miradi itakayotembelewa ni 'Kituo cha Mapato cha Buguruni' na kuonesha Wilaya ya Ilala inavyotumia kwa usahihi TEHAMA kuwahudumia Wananchi ipasavyo chini ya kaulimbiu ya Mwenge isemayo "TEHAMA ni msingi wa Taifa endelevu. Itumie kwa usahihi na Uwajibikaji”.

Karibu Mwenge Maalum wa Uhuru Wilaya ya Ilala, Wilaya iliyobeba sehemu kubwa ya Historia ya Mkoa wa Dar es Salaam, kwa maana ya vivutio na uzuri unaolifanya Jiji la Dar es Salaam kuwa miongoni mwa Majiji 10 yenye mvuto zaidi Barani Afrika, vivutio vilivyopo Ilala ni kama vile; Sanamu ya Askari, Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere, Ikulu ya DSM, Ukumbi wa Karimjee, Bandari ya DSM, Soko la Kariakoo, Viwanja vya Mashujaa Mnazi Mmoja, Kituo cha Reli ya DSM, Hospitali ya Muhimbili, Mnara wa Saa, Hoteli zenye hadhi ya Kimataifa, Soko la Samaki Feri, Benki Kuu ya Tanzania, Boma la Kale, Sekondari ya Pugu, Ukumbi wa Mikutano wa Julius Nyerere

Pamoja na vivutio vyote hivyo kuwepo Wilaya ya Ilala, lakini pia shughuli mbalimbali za kibiashara hufanyika kwenye Wilaya hii inayoongozwa na Mhe. Ludigija, hivyo Ilala imeitambulisha DSM kuwa Jiji mashuhuri kwa biashara

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.