• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Wananchi wahimizwa kula vyakula vya asili

Tarehe iliyowekwa: April 23rd, 2024

Kuelekea maadhimisho ya Miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Halmashauri ya Jiji la DSM kupitia Idara ya Afya imefanya halfa fupi ya kuandaa na kupika Chakula cha asili.

Halfa hiyo imefanyika Leo tarehe 23, Aprili 2024 katika Soko la Kisutu, ambapo mama lishe waliweza kuandaa vyakula vya asili, ikiwa ni mwendelezo wa matukio yanayofanywa na Jiji la DSM kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hii ikiwa ni kuhamasisha wananchi lishe bora kwa kuzingatia makundi 6 ya vyakula.

Akiongea kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya, Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya Ya Ilala Bi. Flora Mgonja amewataka wazazi na walezi wa kuzingatia utoaji wa lishe bora kwa watoto huku akihimiza utumiaji wa vyakula vya asili.

Amesema “Ajenda hii ya Lishe bora ni ajenda ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hivyo Sisi kama Wilaya ya Ilala tunaendelea kutekeleza agizo hilo kwa kutoa elimu ya lishe kwa wananchi kuzingatia lishe bora na ndio maana leo hii ajenda ya lishe imekua moja ya tukio muhimu katika kuelekea maadhimisho ya Sherehe za miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na tumeandaa hafla hii kwaajili ya kuhamasisha ulaji wa mlo kamili huku tukihimiza Watanzania kutosahau asili."

Sambamba na hilo Bi. Mgonja amewapongeza mama lishe wa Soko la Kisutu Kwa kuandaa chakula cha asili kwa kuzingatia taratibu za lishe pamoja na usafi huku akiahidi kulitangaza soko la Kisutu na fursa zinazopatikana kwa wafanyabiashara.

Akiongea katika Hafla hiyo Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Dkt. Zaituni Hamza ameeleza kuwa Idara ya Afya itaendelea kusimamia afua za lishe kama Mhe. Rais anavyosisitiza kwani hakuna maendeleo bila afya bora na afya bora hutokana na ulaji wa lishe bora na mlo kamili.

Kwa upande wake Afisa Lishe wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Bi. Flora Mgimba ameeleza kuwa “Katika kuelekea kilele cha sherehe za miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam tumeandaa hafla ya kutayarisha mlo kamili unaoendana na vyakula asili vya Tanzania hivyo katika hafla hii tumewatumia mama lishe na baba lishe ambao tumewajengea uwezo wa namna ya kuandaa chakula katika hali ya usafi na usalama kwa ustawi wa afya zetu huku tukiendelea kutekeleza Afua za Lishe kama Rais Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyoelekeza."

Naye Mwenyekiti Mama Lishe wa Soko la Kisutu Bi. Pendo Mtiti amewashukuru viongozi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa kuandaa hafla hiyo huku akiahidi kushirikiana na mama lishe wengine kutoa elimu ya lishe kwa wananchi wengine na namna ya kuandaa mlo kamili katika hali ya usafi kwa ustawi wa afya zetu.






Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.