• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

RC Chalamila ajitambulisha rasmi Jiji la Dar es Salaam

Tarehe iliyowekwa: May 30th, 2023

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Mhe.Albert Chalamila leo tarehe 30 Mei, 2023 amefanya kikao maalum na Viongozi pamoja na Watumishi wa ngazi ya Wilaya na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa lengo la kujitambulisha rasmi la kuomba ushirikiano katika utendaji kazi.

Kikao hicho kilichofanyika katika Ukumbi wa mikutano wa Karimjee kilihudhuriwa na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe.Edward Mpogolo, Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya, Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Naibu Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Madiwani, Watendaji wa Kata na Mitaa, Wakuu wa Divisheni na Vitengo na watumishi wa Jiji la Dar es Salaam kutoka kada mbalimbali.

Akiongea na watendaji hao Mhe.Chalamila amewaomba wampe ushirikiano wa kutosha katika kuwatumikia wananchi ili kufanikisha malengo makubwa ya Serikali ya Awamu ya Sita ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Aidha amewasisitiza kupenda kufanya kazi kwa uwazi na kuepuka mambo ya rushwa na kuonea raia kwa kutumia madaraka waliyonayo kuwanyanyasa na kuwanyima haki zao, Amesema “Naomba muwe watu wa kusimamia haki kila wakati, sipendi watendaji ambao wanatumia ujanja ujanja katika kutekeleza majukumu yao. Fanyeni kazi kwa uwazi epukeni rushwa kwa kuwa rushwa ni adui wa maendeleo.”

Mbali na hilo Mhe. Chalamila amewataka watumishi kudumisha ushirikiano baina yao ili kutimiza majukumu yao ipasavyo kwa sababu katika utumishi kila mmoja anafanya kazi kwa kumtegemea mwenzake kwa maslahi mapana ya jamii na nchi yetu kwa ujumla.

Vilevile amewaomba watumishi hao kuendelea kusimamia kwa uadilifu miradi mbalimbali ya maendeleo inayoendelea kutekelezwa katika Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ili Mhe. Rais aweze kuwapatia tena fedha za kuendeleza na kuanzisha miradi mingine mikubwa ya maendeleo. Pia amewataka kusuluhisha kwa wakati migogoro mbalimbali iliyopo katika jamii hasa migogoro ya ardhi kwani baadhi ya migogoro inasababishwa na watendaji wenyewe na kuwaomba waepuke kuwa sehemu ya migogoro iliyopo katika jamii.

Mhe.Chalamila pia amefurahishwa na kampeni iliyokuwepo ya kuwapanga wafanyabiashara ndogondogo katika maeneo rasmi ili kuhakikisha Jiji linakuwa katika hali ya usafi kila wakati na kutoa rai kwa watumishi na viongozi wote kuendelea kuisimamia kampeni hiyo kwa vitendo, na kwamba yeye anaiunga mkono na ataendelea kuisimamia kwa uwekaji wa taa za barabarani ili kupunguza Uhalifu uliokuwepo awali. Vilevile ameahidi kuwa katika uongozi wake hapa Dar es Salaam, atahakikisha mwarobaini wa uchakataji taka ngumu unapatikana.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.