• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Tanga Pharmaceutical and Plastic Ltd watoa Madawati 25 katika Shule ya Msingi Vingunguti

Tarehe iliyowekwa: March 23rd, 2023

Wafadhili kutokaTanga Pharmaceutical and Plastics Limited(TPPL) leo tarehe 23 Machi, 2023 wametoa msaada wa madawati 25 kwa Shule ya Msingi Vingunguti iliyopo Kata ya Vingunguti ikiwa ni sehemu ya mchango wa wadau wa elimu kuhakikisha wanafunzi wote wanasoma katika mazingira bora na tulivu.

Akiongea katika hafla hiyo Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Mhe. Omary Kumbilamoto aliwashukuru wadau hao kwa kutoa kipaumbele katika sekta ya elimu nchini huku akiwaahidi kuendelea kushirikiana nao katika kujenga na kuimarisha sekta ya elimu nchini

“Halmashauri iko tayari kushirikiana na wadau wa maendeleo na nitahakikisha kuwa yote ambayo ni muhimu zaidi yatatekelezwa kwa wakati. Nawashukuru sana wadau kwa kuweza kuwa sehemu ya kuipa kipaumbele elimu Kwani Tanga Pharmaceutical and Plastic Ltd wamekuwa wadau wazuri sana katika kuchangia maendeleo ya Elimu katika Halmashauri yetu kwani leo hii wametoa madawati 25 kwa wanafunzi wa shule ya Msingi Vingunguti huku mwaka 2020 waliweza kuchangia Friji Saba katika Kata ya Vingunguti ambazo zinasaidia katika Shule zetu na Zahanati yetu ya Vingunguti , Kwa hakika nyie ni marafiki wa kweli wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam hatuwezi kuwalipa”.

Sambamba na hilo Mhe.Kumbilamoto aliweza kumkabidhi Cheti cha shukrani Meneja kutoka Tanga Pharmaceutical and Plastic Ltd ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wao katika kuunga mkono sekta ya elimu katika Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam.

Aidha Mhe. Kumbilamoto ametoa wito kwa wazazi na walezi wa watoto wa Shule ya Msingi Vingunguti kuchangia fedha ya chakula kwa watoto wetu kwani Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan amekua akijitoa sana katika kuhakikisha sekta ya elimu inaimarika hivyo kwa kutambua juhudi hizo wazazi wanahitaji nao kuchangia fedha kwa ajili ya chakula kwa wanafunzi ili waweze kusoma kwa bidii wakiwa na afya njema.

Akikabidhi madawati kwa niaba ya wadau hao Meneja Muajiri kutoka Tanga Pharmaceutical Ltd Ndg. Stephen Godfrey amesema “Nina furaha sana kwa kampuni yetu kuwa miongoni mwa wadau wa maendeleo katika kukuza sekta ya elimu nchini hivyo nipende kutoa shukrani zangu za dhati kwa Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa kazi nzuri anayoifanya kwa kuchochea maendeleo katika sekta ya elimu kwani juhudi zake zote ndio zimefanya leo hii sisi kuchangia madawati 25 katika shule ya Vingunguti hivyo niwaombe wanafunzi kusoma kwa bidii ili kukuza ufaulu katika Halmashauri yetu ya Jiji la Dar es Salaam.”

Nae Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Vingunguti Mwl. Mfaume Fadhili amesema “Tunaishukuru sana kampuni ya Tanga Pharmaceutical and Plastic Ltd kwa kuwa mdau wetu mzuri wa maendeleo katika kukuza sekta ya elimu kwani hii leo tunafuraha kupata madawati haya 25 ambapo kwa kiwango chake tumendelea kupunguza idadi ya uhitaji wa madawati katika shule hii ya Msingi Vingunguti yenye jumla ya wanafunzi 2514. Pia tunaishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndani ya miaka hii miwili ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu kwani tuliweza kupata madawati 50."

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.