• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Vijana wapewa wito kuachana na matumizi ya Dawa za Kulevya

Tarehe iliyowekwa: July 5th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Mpogolo amewataka Vijana kuachana na matumizi ya dawa za kulevya na badala yake waungane katika kufanya shughuli halali za kiuchumi ili wajiletee maendeleo katika ngazi ya familia, jamii na hata Taifa.

Mhe. Mpogolo ametoa wito huo leo Julai 05 2024, wakati wa akifunga Kongamano la Vijana la Kapinga Matumizi ya Dawa za Kulevya lililofanyika katika viwanja vya Usikate Tamaa vilivyopo Vingunguti Jijini Dar es Salaam sambamba na kaulimbiu  isemayo ‘WEKEZA KWENYE KINGA NA TIBA DHIDI YA DAWA ZA KULEVYA” ambayo inalenga Serikali, wadau, vijana na wananchi kwa ujumla kuwa na dhamiri ya dhati katika kuwekeza kwenye kinga na tiba ilikupunguza au kuondoa kabisa tatizo la matumizi ya dawa za kulevya hasa kwa vijana kwani kinga na tiba ni uhakika wa ushindi wa mapambano dhidi ya dawa za kulevya.

Akizungumza na vijana pamoja na Wananchi waliohudhuria katika Kongamano hilo Mhe. Mpogolo amesema “Kufuatia wimbi la vijana kuingia katika matumizi ya madawa ya kulevya pamoja na kupata madhara mbalimbali ya kiafya, Serikali imejikita katika kutoa elimu ili jamii ifahamu hivyo Kwa juhudi zinazoendelea za kupambana na matumizi ya madawa ya kulevya, nitoe pongezi na shukrani za dhati kwa kazi kubwa inayofanywa na Uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali ikiwemo MDH, DEH pamoja na Peer to Peer Group katika kuchochea, kuhamasisha na kuratibu shughuli zote za mapambano dhidi ya matumizi ya dawa za kulevya na kuwekeza kwenye kinga na tiba dhidi ya dawa za kulevya. Pia niwasihi vijana wengine ambao hamjaingia kwenye madawa msishawishike kuingia huko na ambao mshaathirika na madawa muendelee kutumia dawa za kuwakinga ili msiathirike zaidi.”

Sambamba na hilo Mhe. Mpogolo amewataka Vijana kuwa na Maadili mema pomoja na kujiepusha na makundi ya ushawishi ili kulinda afya zao na nguvu kazi ya taifa huku akiwataka wajikite zaidi na Shughuli za kimaendeleo pamoja na kuwasisitiza vijana hao kuwa mabalozi wazuri katika kuwaelimisha wale wote ambao hawakupata nafasi ya kushiriki katika kongamano hilo kuhusu athari na madhara ya matumizii ya dawa za kulevya kwa ustawi wa jamii na Taifa kwa ujumla.

“Tunawahimiza kuacha kujihusisha na shughuli zinazokinzana na sheria, taratibu na kanuni za nchi yetu badala yake vijana tutumie mazingira wezeshi tuliyowekewa na Serikali kuongeza ufanisi katika kukuza taaluma, uchumi, elimu na biashara ili kufikia malengo yetu hivyo napenda kuwahakikishia kuwa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya tutaendelea kushirikiana na wadau wote wa vijana kwa kuwawekea mazingira rafiki ili muweze kutekeleza majukumu yenu ipasavyo.” Amesisitiza Mhe. Mpogolo

Katika hatua nyingine Mhe. Mpogolo amewasihi vijana na wananchi wa Wilaya ya Ilala kuhakikisha wanashiriki kikamilifu katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika Oktoba 2024 huku akiwataka kujitokeza kwa wingi katika kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura pindi litakapofunguliwa.

Kwa upande wake Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mhe. Omary Kumbilamoto ameeleza kuwa ni mpango wa Serikali sasa katika kuhakikisha waraibu wote wa matumizi ya dawa za kulevya wanapewa huduma ya matibabu kuanzia ngazi ya zahanati, vituo vya afya na hospitali ambapo kwa sasa Serikali inaboresha kwanza huduma za afya kisha waanze kuratibu mpango huo hivyo amewasihi vijana wa Vingunguti kuhakikisha wana nitoke za kwa wingi kupata tiba na elimu.

Awali akisoma taarifa kwa Mkuu wa Wilaya Mratibu wa Shirika la utoaji elimu juu ya matumizi ya dawa za kulevya (NURGET) Bw. John Samson Busumabu ameeleza kuwa Taarifa ya Dawa za kulevya duniani inaonesha kuwa kumekuwa na ongezeko kubwa la biashara na matumizi ya Dawa za kulevya ambapo hali ya Dawa za Kulevya kwa mwaka 2021 ilionesha kuwa, takribani mtu 1 kati ya kila watu 17 wenye umri kati ya miaka 15 hadi 64 ulimwenguni walitumia Dawa za Kulevya. Katika kipindi cha mwaka uliopita, Idadi iliyokadiriwa ya watumiaji wa Dawa za Kulevya kwa miaka kumi imeongezeka kutoka milioni 240 mwaka 2011 hadi milioni 296 mwaka 2021 ambalo ni ongezeko la asilimia 23%. ambapo Katika kipindi hicho, Dawa za kulevya kama bangi, heroine, metamphetamine, cocaine pamoja na Dawa tiba zenye asili ya kulevya zilitumika. Mwaka 2020, inakadiriwa kuwa watu milioni 36 walitumia Dawa za kulevya jamii ya amphetamine (ATS), milioni 22 walitumia cocaine, na milioni 20 walitumia dawa aina ya “ecstasy” zilizopelekea madhara ya kiafya kwa watumiaji na jamii, kama vile ongezeko la maambukizi ya virusi vya UKIMWI, magonjwa ya akili na homa ya ini hivyo, jitihada mbalimbali zimeendelea kuchukuliwa ili kudhibiti uzalishaji, biashara na matumizi ya Dawa za Kulevya, ikiwa ni pamoja na utoaji wa tiba kwa watu wenye uraibu wa dawa hizo.

Aidha Bw. Busumabu ameeleza kuwa Halmashuri ya Jiji la Dar  es Salaam imeweza kuungana na Wananchi wote Nchini na Duniani kote katika harakati za kudhibiti na kupambana na matumizi ya dawa za kulevya kwani Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam itaendelea kutoa elimu juu ya athari za matumizi ya dawa za kulevya ili kuzuia na kukinga watoto na vijana ambao hawajaingia kwenye matumizi ya dawa za kulevya na kuhakikisha kuwa hawaingii kwenye matumizi hayo huku wakiendelea kusaidiana na Serikali kupitia Mamlaka husika kuhakikisha linazuia uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa Dawa za kulevya nchini ili kuinusuru jamii dhidi ya Dawa za kulevya bila kusahau kuwatambua waraibu wa Dawa za kulevya na kuwaelimisha juu ya huduma za upunguzaji madhara ili kuchangia katika kuwasaidia waathirika wa dawa za kulevya kwa kuwaunganisha na huduma za afya kama kuwapeleka MAT kliniki kwa ajili ya kupata dawa ya maethadone ikiwa ni pamoja na kupata tiba za TB, Homa ya Ini na kupata dawa za ARV kwa walio na maambukizi ya Virusi vya UKIMWI.

Katika Kongamano hilo mada mbalimbali ziliweza kutolewa kwa vijana wapatao 1000 walioshiriki ikiwemo Madhara ya Matumizi ya Dawa za Kulevya ,Haki na Wajibu wa Kijana Kipindi cha Uchaguzi, Fursa za Kiuchumi kwa Vijana, Faida na Hasara ya mitandao ya Kidigitali, jinsi ya kujikinga na maambukizi dhidi ya VVU/UKIMWI pamoja na namna ya kuwa wazalendo na kujitolea kwa Vijana.

















Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.