• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Wilaya ya Ilala yaweka Mikakati ya Kudhibiti Magonjwa ya Mlipuko

Tarehe iliyowekwa: November 7th, 2023

Wilaya ya Ilala yaweka mikakati ya kudhibiti Magonjwa ya Mlipuko katika Jamii. Hayo ameyabainisha Mkuu wa Wilaya ya Ilala leo Novemba 7, 2023 wakati akizindua mpango wa ugharibishaji wa huduma za chanjo ya magonjwa ya mlipuko katika Ukumbi wa Meya uliopo Arnatoglou Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Mkuu wa Wilaya ya Ilala  Mhe. Edward  Mpogolo amesema "Tumeandaa utaratibu mzuri wa kupambana na adui wa afya kwani mpango huu wa uwezeshaji Jamii kutambua changamoto za kiafya na kuweka mikakati ya kukabiliana na changamoto hizo utafanyika kwa asilimia mia katika tarafa zetu za Segerea na Ukonga hivyo niwashukuru wadau wetu TIP na UNICEF kuwezesha chanjo hii pia niwaahidi tutasimamia kwa ukaribu zaidi zoezi hili na baada ya hapo tutafanya tathmini."

Sambamba na hilo Mhe. Mpogolo ameendelea kusema mpango huu umekua darasa zuri kwa Wilaya ya Ilala kusimamia miradi mingine hivyo kufanya mabadiliko kwenye sekta ya afya huku akihimiza kushirikiana na jamii ili kupata matokeoya chanjo kwa asilimia mia.

Akitoa Shukrani zake wakati wa uzinduzi huo Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam Ndg. Jomaary Satura ameahidi kutekeleza yote yaliyoelekezwa huku akieleza kuwa Halamashauri ya Jiji la Dar es Salaam kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri itaendelea kuboresha huduma za afya na kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya na kwa wakati sahihi.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Dkt. Zaituni Hamza ameeleza kuwa “Uzinduzi wa chanjo hii ni mkakati wa kutokomeza magonjwa ya mlipuko hivyo tunaomba kushirikiana na viongozi wetu kuhakikisha mnasimamia Agenda ya Mheshimiwa Rais ya kutokomeza magonjwa ya mlipuko hasa kipindi hichi cha mvua hivyo tuhakikishe wananchi wanapata chanjo ya mlipuko ili kukabiliana na magonjwa ya milipuko pindi yanapotokea."

Naye Afisa Programu sehemu ya elimu ya afya kwa umma kutoka Wizara Afya Bw. Simon Nzilibili ameeleza kuwa afua ya uraghibishaji wa huduma za chanjo kwa viongozi wa kijamii imelenga kuhamasisha matumizi endelevu ya huduma za chanjo kwa watoto chini ya miaka 5 ambao hawajapata chanjo au hawajakamilisha chanjo ndani ya Wilaya ya Ilala walau asilimia 50 hadi Mwezi Desemba, 2023 kupitia mpango wa uwezeshaji jamii kutambua changamoto za kiafya na kuweka mikakati ya kukubaliana na changamoto hizo ambapo kwa Wilaya ya Ilala mpango huo utahusisha mitaa 131 ndani ya Tarafa za Ukonga na Segerea (70 Ukonga, 61 Segerea), WAJA 189 pamoja na wahudumu wa afya 189 huku jumla ya familia 259,200 sawa na asilimia 56.5 ya familia zote 458,614 zilizopo Wilaya ya Ilala zinatarajiwa kufikiwa.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.