• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

DC Ilala amshukuru Rais Samia kwa fedha za ujenzi wa Soko la Kariakoo

Tarehe iliyowekwa: July 13th, 2022

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mhe. Ng’wilabuzu Ludigija leo tarehe 13 Julai, 2022 amefanya ziara ya kukagua ukarabati na ujenzi wa Soko Kuu la Kariakoo, kwa lengo la kuona namna hatua za ujenzi huo unavyoendelea sambamba na matarajio ya kukamilika kwa mradi huo. Ukarabati wa soko hilo umetokana na ajali ya  moto iliyotokea miezi kadhaa iliyopita na kusababisha hasara kwa kuteketeza mali zilizopo.

Aidha, ukarabati huo unaenda sambamba na ujenzi wa Soko Dogo lililopo pembeni ya Soko Kuu la Kariakoo. Akiongea katika ziara hiyo Mhe. Ludigija amesema “Namshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa, Samia Suluhu Hassan, kwa kutoa fedha ambazo zinatumika katika ujenzi wa soko dogo na ukarabati wa soko kuu la kariakoo, shilingi Bilioni 28 Rais wetu amezitoa kukamilisha ujenzi huu, ikiwa Bilioni 26 kwa ajili ya Mkandarasi na Shiling Bilioni 2 kwa ajili ya Mshauri wa Ujenzi huu ambao ni Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), hii inaonesha namna Rais anajali wafanya biashara katika soko hili”.

Katika ziara hiyo Mhe. Ludigija aliambatana na wafanyabiashara pamoja na viongozi wa Soko Dogo na Soko Kubwa la Kariakoo na viongozi wa wamachinga kwa madhumuni ya kuja kuangalia ujenzi unavyoendelea na kuzidi kuwa na imani na Serikali juu wafanyabiashara wote kurejea pindi soko litakapomalizika.

“Napenda kuwahakikishia kwamba wafanyabiashara wote kuwa na usawa katika biashara kutokana na ukweli kwamba kuna wafanyabiashara wengi wamepisha ujenzi pamoja na ukarabati huu, hivyo basi wote muwe na subira na mtakuwa kipaumbele cha kwanza kurudi katika soko hili kama mwanzo ili mfanye biashara zenu bila ya wasiwasi”.

Sambamba na hilo, Mkuu wa Wilaya hiyo, alitoa wito kwa wafanyabiashara wadogowadogo maarufu kama Machinga kuacha mara moja kurudi katika maeneo ambayo siyo rasmi kwa wafanyabiashara na kuwasihii watengezaji wa simu za mkononi kutozuia Barabara za watembea kwa miguu.

Ujenzi na ukarabati wa soko kuu la Kariakoo mpaka sasa umefikia asilimia 28% ya ujenzi ikiwa unatarajiwa kumalizika mnamo Agosti, 2023 akieleza Mkandarasi wa Ujenzi huo Ndugu, Johnson Nyamwelu, amesema “katika nafasi yetu kama wakandarasi kwanza tunaunga mkono Serikali ya awamu ya Sita sambamba na kusimamia ujenzi huu ambao kwa sasa unaenda vizuri malengo yetu kumaliza kabla ya wakati ili kumheshimisha Rais wetu kwa utekelezaji bora wa ujenzi huu”

Ukarabati wa Soko Kuu la Kariakoo unatarajiwa kuboreshwa zaidi ukitofautisha na ulivyokuwa awali ikiwa maboresho zaidi katika kuongeza sehemu za biashara za mabenki, uwekwaji wa lifti, kuongeza maeneo zaidi ya wafanya biashara wadogo na wakubwa ikiwa ni dhamira ya kuweza kuwarudisha wote waliopisha ujenzi na ukarabati kurudi na kuendelea kufanya biashara kama awali.

Ziara hiyo ilihitimishwa kwa Mkuu wa Wilaya kuweza kutembelea Soko Kuu la Kisutu na kuweza kuongea na wafanyabiashara wa soko hilo ili kusikia kero zao pamoja na kutafuta njia ya upatikanaji wa suluhisho, sambamba na kuwsikiliza wafanya biashara katika soko dogo la Uuzaji wa Kuku.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.