• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Jiji la Dar es Salaam lavuka lengo katika utoaji wa Chanjo ya Polio

Tarehe iliyowekwa: May 26th, 2022

Chanjo ya polio ni chanjo ambayo inatolewa kwa ajili ya kujikinga na virusi vya polio. Virusi hivi ni kati ya virusi ambavyo vinaleta ugonjwa wa kupooza, hivyo kusababisha mtu kushindwa kutembea, kuendelea na shughuli zake za kila siku na huathiri zaidi watoto walio na umri wa chini ya miaka mitano.

Nchini Tanzania Serikali kupitia Wizara ya Afya iliendesha kampeni ya chanjo ya polio kwa watoto walio na umri wa chini ya miaka mitano. Kampeni hiyo ilianza tarehe 18 Mei hadi 21 Mei, 2022.

Kampeni hii ilifanyika hapa nchini kutokana na maelekezo ya Shirika la Afya Duniani baada ya kubainika kuwepo kwa virusi vya polio nchini Malawi na kufanya mataifa ya jirani na  nchi hiyo ikiwemo Tanzania kupata chanjo ya kujikinga dhidi ya ugonjwa huo.

Katika Jiji la Dar es Salaam, Mganga Mkuu wa Jiji la Dar es Salaam, Dr. Elizabeth Nyema, ametoa tathimini ya zoezi zima la utoaji wa chanjo na kusema kuwa katika kipindi cha siku nne za kampeni ya utoaji wa chanjo hiyo walitarajia kutoa chanjo kwa jumla ya watoto 221,201.

Alisema kuwa hadi kampeni hiyo ilipomalizika walifanikiwa kutoa chanjo kwa jumla ya watoto 266,908 ambayo ni sawa na asilimia 121. Hivyo kwa upande wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imefanikiwa kwa kiasi kikubwa katika zoezi hilo kwani muitikio wa wananchi ulikuwa ni mkubwa.

Dr. Nyema alisema kuwa hata baada ya kumalizika kwa siku nne za kampeni hiyo bado kuna baadhi ya wananchi waliojitokeza kuomba wapate chanjo hiyo kwa kuwa hawakufanikiwa kufikiwa na watoa huduma katika siku zile nne za kampeni. Kutokana na sababu hii Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam iliendelea kutoa chanjo hiyo kupitia vituo vyake vyote vya afya.

Dr. Nyema alisema kuwa wanawakinga watoto walio na umri wa chini ya miaka mitano kwa sababu katika umri huo huwa hawana kinga za kutosha ukilinganisha na wale wenye umri zaidi ya huo.  Chanjo hiyo husaidia kuwakinga watoto wa rika hiyo ili wasipate maambukizi ya magonjwa mbalimbali ikiwemo ugonjwa wa polio.

Aidha, amewahakikishia wananchi wa Jji la Dar es Salaam kuwa chanjo zote zinazotangazwa na kutolewa na Serikali zimefanyiwa utafiti wa kina na ziko salama. Amewataka wananchi kujitokeza kupata chanjo hizo kwa wakati kwa ajili ya kujikinga na magonjwa mbalimbali hasa magonjwa ya mlipuko.

Dr. Nyema amewapongeza wananchi wote wa Dar es Salaam kwa kuendelea kufuata taratibu za afya na kutoa wito kuwa wahakikishe pale ambapo Serikali inatangaza kampeni mbalimbali waweze kuwa na mwitikio chanya na kujitokeza kwa wingi kwa ajili ya kupata chanjo hizo.

Amesema, “Tumetoka kwenye chanjo ya polio, tunaendelea na chanjo ya UVIKO 19 lakini pia kuna chanjo zile za watoto chini ya miaka mitano zinazoendelea vituoni, wananchi wahakikishe wanawafikisha watoto kupata chanjo hizo ili kuwakinga na magonjwa mbalimbali.”

Kampeni ya utoaji wa chanjo ya polio katika Jiji la Dar es Salaam ilitekelezwa kwa wataalamu wa afya kupita nyumba kwa nyumba, kwenye maeneo ya shule za watoto, masoko, maeneo ya mikusanyiko mikubwa ya watu na kwenye vituo vya kutolea huduma za afya. Hivyo, zoezi la utoaji wa chanjo hii lilifanikiwa kwa kiwango kikubwa kutokana na mwitikio mkubwa wa wananchi.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.