• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Jiji la DSM kushirikiana na Ubalozi wa China Nchini Tanzania kuboresha Sekta ya Elimu

Tarehe iliyowekwa: March 20th, 2024

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Dar es Salaam Ndugu Abbas Mtemvu ameushukuru Ubalozi wa China nchini Tanzania kwa kuendelea kuunga mkono jitihada mbalimbali zinazofanywa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuinua sekta ya Elimu nchini.

Mtemvu ameyasema hayo wakati wa Hafla ya kukabidhi viti na meza 80 vyenye thamani ya shilingi Mil.7.3 zilizogawiwa katika shule za Msingi na Sekondari za Jimbo la Ilala  pamoja na vifaa vya michezo vilivyogharimu shilingi Mil.24 vilivyotolewa na Serikali ya watu wa China kupitia kwa balozi wake Chen Mingjian iliyofanyika tarehe 20 Machi 2024 katika viwanja vya Karimjee Jijini Dar es Salaam.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Ilala ambaye pia Ni Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amesema kuwa vifaa hivyo walivyokabidhiwa ni namna mojawapo ya kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuinua sekta ya Elimu na michezo nchini na kuongeza kuwa misaada hiyo sio tu itaimarisha ushirikiano baina ya Jimbo la Ilala na Ubalozi wa China bali na Serikali ya Tanzania na China.

Awali akiongea katika hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Mpogolo ameeleza kuwa “Nipende kuwashukuru wenzetu kutoka Serikali ya China kupitia ubalozi wa China Nchini Tanzania kwa kuendelea kushirikiana nasi katika kuhakikisha uboreshaji wa elimu kwenye Jiji letu la Dar es Salaam hadi kutoa viti na meza 80 kwa Walimu wa Shule za Msingi na Sekondari. Hivyo tunaahidi kushirikiana na wenzetu wa China katika kuhakikisha tunakuza Sekta ya Elimu nchini kwa kuwapatia Wanafunzi elimu bora pamoja na kutengeza mazingira rafiki ya kufundishia pia nitoe wito kwa Walimu waliokabidhiwa viti na meza hizi kuhakikisha wana vitunza ili viweze kudumu kwa muda mrefu”.

Naye Balozi wa China nchini Tanzania, Chen Mingjian, amesema kuwa Serikali ya China itaendeleza urafiki na ushirikiano mzuri baina ya Jimbo la Ilala na Tanzania kwa ujumla kwa kuboresha maisha ya Watanzania na maendeleo ya vijana.

Aidha, viti na meza hizo zitagawanywa katika Shule 16 za Jimbo la Ilala zikiwemo shule 8 za Msingi na 8 za Sekondari huku vifaa vya michezo vikipelekwa katika Kata za Jimbo la Ilala kwaajili ya mashindano ya Ilala Super Cup.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.