• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Jiji la DSM lapitisha Rasimu ya Mpango na Bajeti ya Shilingi Bilioni 218.2 kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

Tarehe iliyowekwa: February 10th, 2023

BARAZA la Madiwani Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, leo Tarehe 10 Februari, 2023limefanya Mkutano Maalum wa Mapitio ya Mpango na Bajeti ya Mwaka 2022/2023 kwa kipindi cha nusu mwaka (Julai-Desemba, 2022) na kufanya Makadirio ya Mpango na Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2023/2024 wenye Jumla ya Shilingi Bilioni 218.2, ambapo kati ya fedha hizo kiasi cha Shilingi Bilioni 90.7 sawa na 41.56% ya Bajeti yote ni makusanyo kutoka vyanzo vya mapato ya ndani ya Halmashauri na Shilingi Bilioni 127.5 sawa na 58.43% ya Bajeti ni fedha za Ruzuku kutoka Serikali Kuu ambazo ni kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo na Matumizi ya kawaida.

Aidha, kikao hicho kilichofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa Arnatouglou na kuongozwa na Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mhe. Omary Kumbilamoto, kilipokea, kikajadili na kisha kupitisha Rasimu ya Mpango na Bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024 ambapo Bajeti ya Mapato ya ndani ya Halmashauri imeongezeka kwa 10.7% ukilinganisha na Bajeti ya Shilingi Bilioni 80 ya mwaka 2022/2023, hii imetokana na mikakati bora iliyowekwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwenye ukusanyaji wa mapato na uibuaji wa vyanzo vipya vya mapato. Katika Makadirio ya Mpango na Bajeti ya mwaka 2023/2024 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imeweka Mikakati Saba (07) itakayosaidia kufanikisha ukusanyaji wa mapato ya ndani ya Halmashauri ili iweze kutekeleza Rasimu ya Mpango na Bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024 kwa asilimia 100, pamoja na kuwa na Vipaumbele Kumi (10) vya Mpango na Bajeti.

Makadirio ya Mapato ya Ndani ya Halmashauri kwa mwaka 2023/2024

Akisoma taarifa kuhusu makadirio ya mpango na bajeti ya mwaka 2023/2024 mbele ya

Baraza la Madiwani, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Injinia Amani Mafuru alisema "Kwa mwaka wa fedha 2023/2024 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imepanga kukusanya Shilingi Bilioni 90.7 kutoka kwenye vyanzo vyake vya ndani"


Matumizi ya Mapato ya ndani ya Halmashauri kwa mwaka 2022/2023

"Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa mwaka wa fedha 2023/2024 kwenye Mapato yake ya Ndani inatarajia kutumia fedha kiasi cha Shilingi Bilioni 90.7 katika mchanganuo ufuatao; Matumizi Mengineyo Shilingi Bilioni 20.5 sawa na 22.6% ya Bajeti, Miradi ya Maendeleo Shilingi Bilioni 47.9 sawa na 52.8% ya Bajeti na Vyanzo Fungiwa Shilingi Bilioni 22.3 sawa na 24.5% ya Bajeti" alisema Injinia Mafuru

Makadirio ya fedha za Ruzuku kutoka Serikali Kuu

Ruzuku ya Shilingi Bilioni 127.5 kutoka Serikali Kuu imegawanywa katika maeneo mawili ambayo ni Matumizi ya Kawaida na Miradi ya Maendeleo

Mchanganuo wa Matumizi ya kawaida kwa fedha ya Ruzuku

"Kwa mwaka wa fedha 2023/2024 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam inatarajia kutumia Shilingi Bilioni 107.3 ya fedha ya ruzuku sawa na 84.1% kulipa Mishahara na Shilingi Bilioni 1.36 sawa na 1.06% kwa ajili ya Matumizi Mengineyo" alisema Injinia Mafuru


Mchanganuo wa fedha za Miradi ya Maendeleo kwa fedha ya Ruzuku

Katika kipindi kijacho cha 2023/2024 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imepanga kutumia Shilingi Bilioni 18.6 kutekeleza Miradi ya Maendeleo ambayo ni sawa na 14.5%. Katika kuandaa Rasimu ya Mpango na Bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imezingatia Mwongozo wa uandaaji wa Bajeti uliotolewa na Hazina Mwezi Desemba 2022, Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020 hadi 2025, Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, aliyoitoa Bungeni.

Sambamba na hayo, lakini pia uandaaji wa Rasimu ya Mpango na Bajeti umezingatia Sheria ya Bajeti Na. 11 ya mwaka 2015 sura 439 pamoja na kanuni zake, Mkakati wa Taifa wa Mapambano dhidi ya rushwa awamu ya Tatu, Malengo ya Maendeleo Endelevu, Mpango wa Mkakati wa Taifa wa kukuza uchumi na kupunguza umasikini Tanzania (MKUKUTA) II , Maoni ya wadau mbalimbali wa Halmashauri ambao wameshiriki katika maandalizi ya bajeti hii kuanzia ngazi ya Mtaa, Kata, Idara hadi Halmashauri kwa ujumla kwa kutumia mfumo wa Fursa na Vikwazo (O & OD iliyoboreshwa).

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.