• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Jiji la DSM latekeleza agizo la Waziri Kairuki kwa Shule ya Kifuru, DCB yachangia madawati 30

Tarehe iliyowekwa: March 9th, 2023

Katika kutekeleza agizo la Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) Mhe. Angellah Kairuki wakati wa ziara yake alipotembelea Jimbo la Segerea katika shule ya Msingi Kifuru mnamo tarehe 1, Machi 2023 aliagiza Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kuhakikisha wanaleta madawati 500 kwa wanafunzi wa kifuru.

Hivyo Katika kutekeleza agizo hilo, leo Machi 09, 2023 Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam kwa Kushirikiana na Mkurugenzi wa DCB Bank wameweza kukabidhi madawati 500 kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Kifuru.

Akikabidhi Madawati hayo Mkurugenzi wa DCB Bank Ndg. Isdory Msaki ameeleza kuwa “Katika kutambua jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kukuza na kuendeleza sekta ya Elimu Nchini sisi kama DCB tumekuja na kauli mbiu isemayo ‘Elimu Mpango Mzima na Mama’ ambayo inalenga kuhamasisha suala zima la elimu nchini kwa watoto wetu hivyo tuhakikishe tunatumia vyema fursa ya elimu bure na kuwapeleka watoto wetu shuleni kupata elimu bora.”

Sambamba na hilo Ndg. Msaki amewataka wanafunzi wa Shule ya Msingi Kifuru kusoma kwa bidii kwani jamii inatambua umuhimu wa elimu na ndiyo maana Bank ya DCB imeweza kuchangia madawati kwaajili ya kuwasaidia wanafunzi hao kusoma katika mazingira bora na salama.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam Eng. Amani Mafuru amesema “Napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa Bank ya DCB kwani Waziri wa OR-TAMISEMI alipotoa maagizo ya kuleta madawati katika Shule hii tuliongea na Mkurugenzi wa DCB na yeye kama mdau wetu aliweza kutusaidia madawati 30 ambayo leo hii tumeweza kukabidhiwa hivyo nipende kusema yote tuliyoagizwa na Mheshimiwa Waziri kuyatekeleza tutayatekeleza ipasavyo hatua kwa hatua na tumeanza na hili.”

Sambamba na hilo Eng.Mafuru amewataka wanafunzi kusoma kwa bidii kwani hayo yote yanatekelezwa ili kuwajengea wao mazingira rafiki ya kusoma na kupata elimu bora.

Akitoa neno la shukrani kwa niaba ya wanafunzi wengine Dada Mkuu wa Shule ya Msingi Kifuru Sarah Edwine amesema “Namshukuru Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutujengea madarasa, pia napenda kumshukuru Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam pamoja na Mkurugenzi wa Bank ya DCB kwa kutekeleza agizo la Waziri wa TAMISEMI Mheshimiwa Kairuki na kutuletea madawati kama walivyoagizwa hivyo niwaahidi tutasoma kwa bidii na tutafaulu kwa kiwango cha juu zaidi kama mlivyotutekelezea hili na sisi tunaenda kuongeza ufaulu katika Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa Shule za Msingi.”

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.