• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Ilala watembelea Idara ya Afya Jiji la DSM

Tarehe iliyowekwa: January 19th, 2023

Idara ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii, imetoa elimu kwa wajumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi ya CCM Wilaya ya Ilala, ambapo Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Dkt. Elizabeth Nyema, amewashauri wajumbe wa kamati ya utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi ya CCM Wilaya ya Ilala kupeleka Elimu ya Afya kwa wananchi wa Ilala.

Hayo ameyabainisha leo, wakati walipofanya kikao cha majadiliano baina ya wajumbe wa kamati ya utekelezaji ya Jumuiya ya wazazi ya CCM Wilaya ya Ilala pamoja na Idara ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam.

"Wakina Mama wengi huanza kliniki wakiwa na mimba ya wiki kumi na mbili na wengine wanakuja wakiwa wanakaribia kujifungua kwahiyo hata kama kuna tatizo nyuma hatuwezi kuligundua wakati mtoto ameshakua na kama hajapata dawa za awali kuweza kumkinga yeye na mtoto ikiwemo malaria inakuwa ni changamoto kwaiyo unakuta mama dakika za mwisho anapoteza mtoto lakini ni kwa sababu hakufika kliniki kwa wakati, tunaomba pia hii elimu iweze kufika ili iweze kuwasaidia akina mama na kupunguza vifo vya mama na mtoto" Alisema Dkt. Elizabeth Nyema.

Awali Katibu wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ilala, Ndugu Mtiti Mbassa Jirabi, alieleza kuwa eneo la Afya ni eneo ambalo limepewa kipaumbele katika kamati ya Wazazi ya Wilaya na kusisitiza Sekta ya Afya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kuendelea kuwapatia elimu ili kuwawezesha nao kuisaidia Jamii

"Naomba nilisisitize hilo kama Sekta ya Afya itakuwa na utaratibu wa aina hiyo kutupatia elimu, sisi tunahitaji elimu kutoka kwenu ili tuweze kusaidia hizi jamii." alisema Jirabi

Aidha, Walter Kayombo, ambaye ni Mratibu wa Mfuko wa Afya ya Jamii (iCHF) Jiji la Dar es Salaam, alisema mwaka juzi walitenga milioni 6.4, kwaajili ya kuhudumia makundi maalumu yanayohusisha wazee, watu wenye ulemavu na wananchi wa kawaida wasio na uwezo wa kuhimili changamoto za matibabu, katika kiasi hicho cha milioni 6.4 kilichokuwa kimetengwa waliweza kutoa kadi 125 za utambuzi kwa wazee maeneo tofauti tofauti kwenye Halmashauri.

Naye Mratibu wa Malaria Jiji la Dar es Salaam, Ally Adinani, alisema kuwa lengo lao kubwa ni kupunguza Mbu waenezao malaria katika Jiji la Dar es Salaam  "Tuna mbu ambao ni wengi na asilimia kubwa karibu 96% ni ‘curisense’ ambao ni mbu wasumbufu ambao wanaeneza mabusha na matende na 4% ni mbu wa malaria ambapo ukiangalia kimsingi wengi wako kwenye maeneo ya nje ya Jiji la Dar es Salaam" alisema AdnanI

Hata hivyo, Ndg. Adinani ametoa ufafanuzi kuwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imepanga bajeti ya ununuzi wa viua mbu kwa mwaka huu kudhibiti maambukizi ya malaria katika Jiji la hilo.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.