• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Wataalam Dar wajipanga kutekeleza mpango mpya wa mabadiliko ya tabianchi

Tarehe iliyowekwa: December 1st, 2022

Katika jitihada zinazoonekana kuwa na mafanikio makubwa katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, Jiji la Dar es Salaam kwa kushirikiana na Umoja wa Majiji Duniani, C40 Cities, linatarajia kuanza rasmi utekelezaji wa mpango wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi katika Jiji la Dar es Salaam ulioandaliwa na Mamlala za Serikali za Mitaa katika Jiji la Dar es Salaam kwa kushirikiana na C40 Cities na wadau mbalimbali.

Akifungua warsha ya siku mbili ya wataalam katika sekta ya mabadiliko ya tabianchi iliyoanza Disemba 1, 2022 katika Ukumbi wa Mikutano wa hoteli ya Holiday Inn jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi wa Jiji  la Dar es Salaam Joshua Muhogolo amesema kuwa mpango huo ni sehemu ya juhudi za Serikali za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi katika Jiji la Dar es Salaam.

Muhogolo amewataka washiriki wa warsha hiyo kutumia fursa hiyo kuongeza ujuzi wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kwa manufaa ya umma.

Baadhi ya washiriki waliofika kwenye warsha hiyo

"Nimejulishwa kwamba C40 Cities itaendelea kutoa mafunzo zaidi kupitia warsha kama hii, ninawataka mtumie fursa hizi kwa manufaa ya umma kwa kufanikisha malengo ya Serikali katika Jiji la Dar es Salaam dhidi ya mabadiliko ya tabianchi" alisema Muhogolo.

Kwa upande wake mwakilishi wa C40 Cities ambaye ni mshauri wa masuala ya mabadiliko ya tabianchi, Jophillen Bejumula, ametoa wito kwa washiriki wa warsha hiyo kuunganisha nguvu ili kufanikisha utekelezaji wa mpango huo ambao utasaidia kutatua changamoto zinazosababishwa na mabadiliko ya tabianchi na kuzuia athari zaidi zinazoweza kusababishwa na mabadiliko ya tabianchi.

Warsha hiyo iliyoandaliwa na C40 Cities imewaleta pamoja wataalam kutoka katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Manispaa ya Ubungo, Kinondoni, Kigamboni na Temeke kutoka katika sekta ya udhibiti taka, fedha, mipango, ardhi, maendeleo ya jamii, kilimo na ushirika, biashara viwanda na uwekezaji.

C40 Cities ambayo ni umoja wa zaidi ya majiji 97 Duniani imekuwa ikishirikiana na Halmashauri ya Jiji za Dar es Salaam kwa zaidi ya miaka saba katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi ikiwajengea uwezo wataalam wa Dar es Salaam kwa kuwapatia mafunzo ndani na nje ya nchi ili kufanikisha adhma ya Serikali katika Jiji la Dar es Salaam ya kupambana na janga la mabadiliko ya tabianchi

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.