• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Waziri Mkuu aelekeza Afua zote za Ugonjwa wa Malaria Kusimamiwa Vizuri ili kuweza kutokomeza kabisa Malaria Nchini

Tarehe iliyowekwa: April 25th, 2023

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na wadau wa Sekta ya Afya imepiga hatua kubwa kwenye mapambano dhidi ya ugonjwa wa malaria Nchini, hayo yamebainishwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Majaliwa Kassim Majaliwa leo Aprili 23, 2023 kwenye maadhimisho ya Siku ya Malaria Duniani ambayo Kitaifa yamefanyika Jijini Dar es Salaam katika viwanja vya Mnazi Mmoja.

“Tumepiga hatua kubwa kwenye mapambano dhidi ya Ugonjwa wa Malaria, tumeweza kupunguza kiwango cha maambukizi kutoka asilimia 14.8 mwaka 2015 hadi kufikia asilimia 8.1 mwaka 2022." amesema Waziri Mkuu Majaliwa.

Mhe. Majaliwa amesema kauli mbiu ya maadhimisho ya siku ya malaria duniani kwa mwaka huu ambayo ni ‘Wakati wa kutokomeza Malaria ni sasa, Badilika, Wekeza, Tekeleza. Ziro Malaria inaanza na Mimi’ itekelezwa kwa vitendo kwa kuwa inaenda sambamba na utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ibara ya 83 (M,N,O) ya utekelezaji wa mkakati wa Serikali kwenye Mapambano dhidi ya Malaria.

“Ilani ya Chama Cha Mapinduzi imetoa maelekezo kwa Serikali, kuendelea kuihamasisha jamii juu ya matumizi ya vyandarua vilivyowekwa dawa, kupulizia viuwatilifu ukoko kwenye nyumba, kutekeleza mpango wa kuangamiza viluilui vya mbu na kutoa hamasa katika mapambano dhidi ya magonjwa ya kuambukiza” ameeleza Waziri Mkuu.

Aidha katika maadhimisho hayo Mhe. Majawiliwa amezindua gari maalumu litakalotumika katika shughuli mbalimbali za utafiti juu ya ugonjwa wa Malaria pamoja na Uzinduzi wa baraza la kupambana na Malaria lenye wajumbe 19 huku akiwasisitiza kuhakikisha wanafanya kampeni za kudhibiti ugonjwa huo kwa kuanza na Mikoa ambayo iko chini ya asilimia moja ili kutokomeza kabisa ugonjwa huo.

Katika kutelekeza kwa Vitendo mapambano dhidi ya ugonjwa wa malaria, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa amesema kuwa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ametoa unafuu kwa watanzania kwa kupata huduma za tiba ya ugonjwa wa malaria bure, ikiwemo Vipimo vya MRDT, Dawa za Aru, Sindano ya Malaria kali, Dawa za SP kwa ajili ya kutibu Malaria kwa wajawazito vyote vitatolewa bure kuanzia sasa.

Kwa upande wake Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amesema Serikali imeendelea na mapambano dhidi ya kutokomeza ugonjwa huo na hadi kufikia mwaka 2022, idadi ya Mikoa yenye kiwango cha maambukizi ya malaria chini ya asilimia moja imefikia 9 (Arusha, Kilimanjaro, Manyara, Dodoma, Singida, Iringa, Dar es Salaam, Songwe na Mwanza) kutoka Mikoa 6 mwaka 2017 hivyo kufanya asilimia ya watu wanaoishi katika maeneo yenye malaria chini ya asilimia moja kufikia asilimia 41.

Sambamba na hilo Mhe. Ummy amesema Serikali kupitia Wizara ya Afya imeweka kipaumbele kikubwa kwenye mapambano ya kutokomeza ugonjwa wa Malaria ifikapo Mwaka 2030 hivyo ni vyema Wadau wa Sekta ya Afya kwenye mapambano dhidi ya Malaria wakaunganisha nguvu za pamoja na Serikali katika utekelezaji wa afua za mapambano dhidi ya ugonjwa huo na kuweza kuutokomeza nchini.

Akitoa Shukrani zake kwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Amos Makalla amesema “Tunamshukuru Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa fedha zaidi ya bilioni 37 kwaajili ya kuboresha huduma za Afya katika Mkoa wa Dar es Salaam kwani fedha hizo zimetumika katika kujenga Zahanati, vituo vya Afya pamoja na kuboresha huduma mbalimbali katika Hospitali za Wilaya ambazo zinaendana na kasi za utokomezaji wa ugonjwa wa malaria pia tunashukuru kwani Wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam wameweza kupata elimu ya jinsi ya kujikinga na Malaria ambapo Mkoa wa Dar es Salaam umeweza kupunguza maambukizi ya ugonjwa wa malaria kwa asilimia kubwa kutoka asilimia 6% Mpaka kufikia 0.9% za maambukizi hii inatokana na kampeni ya ‘Safisha Pendezesha Dar es Salaam’ ambayo imeonesha mafanikio makubwa kwani Wananchi wamekua wakisafisha mitaro ya maji, kufyeka majani, kiziba madimbwi ya maji bila kusahau kulala kwenye chandarua hivyo naamini Mkoa wa Dar es Salaam utakua wa kwanza kutokomeza ugonjwa wa Malaria Nchini”.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.