• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Waziri Mkuu Majaliwa atembelea machinjio ya Vingunguti

Tarehe iliyowekwa: May 17th, 2021

Na: Judith Damas

Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa  amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam kuhakikisha kuwa hadi kufikia Juni 30 , 2021 Machinjio ya  kisasa ya Vingunguti ianze kufanya kazi ili kuhakikisha tunapata nyama yenye thamani zaidi ambayo itauzwa hadi nje ya Nchi ya Tanzania.

Ameyasema hayo wakati akizungumza na wananchi wa kata ya Vingunguti katika ziara yake ya kikazi ya kukagua maendeleo ya mradi wa Machinjio ya kisasa ya Vingunguti leo Mie17,2021 Waziri Mkuu ameeleza kuwa mradi huo umekamilika kwa asilimia 95 ikiwemo ujenzi wa visima vya kuchuja maji taka, vyumba vya kuhifadhia nyama pamoja na chumba cha kuchomea mizoga hivyo kumuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam kuhakikisha kuwa Marekebisho madogomadogo yaliyosalia  kukamilika katika machinjio hayo  ili yaanze kufanya kazi rasmi.

Sambamba na hilo Waziri Mkuu amemwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam kuhakikisha wanaziba mifereji ya maji  na kujenga mifereji maaulum yakupitisha maji ili kuzuia maji kutiririka na kuharibu miundombinu ya na mikazi ya  watu.

" Niwaagize Jiji kuhakikisha kuwa wanajenga mifereji maalumu ya kupeleka maji mtoni na hivyo kwenye hizo asilimia tano(5)zilizobaki  mjenge mifereji hiyo ili kuhakikisha maji yanaenda mtoni  na sio kwenye mikazi  ya watu". Amesema Waziri Mkuu.

Aidha Waziri Mkuu amemwelekeza Mwenyekiti wa wajasiriamali kwenye machinjio hayo kuhakikisha   wananashirikiana na Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam ili kuweza kumaliza tofauti zao na kuzungumza lugha moja.

"Ningetamani sana kama tungeweza kuanza kutumia machinjio haya ya Kisasa hata leo  lakini pia mwenyekiti wenu ameniambia ni vyema tukamilishe kwanza ujenzi huu, ila na mimi ningewaomba mshirikiane na Halmashauri ya Jiji ili muweze kuwa kitu kimoja ili kuweza kufanikisha jambo hili na pia muda mwingine mnaweza kutafuta ngo'mbe na kuja kuchinja huku ili kuwafanya wachinjaji kuzoea na mara baada ya kuanza kutumia machinjio haya ya kisasa ya Vingunguti kazi ziwe zinaenda kwa uharaka zaidi"

Vilevile, Waziri Mkuu  amemuhakikishia Mbunge wa Jimbo la segerea kuwa suala la ajira kwa vijana waliopo maeneo ya machinjio hayo amelipokea moja kwa moja na anamuachia Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam atakapotangaza ajira aanze na vijana hao wanaofanya kazi katika machinjio ya zamani kwani wanauzoefu mkubwa  zaidi.

Kwa upande wake Naibu waziri wa Ardhi Mhe.Anjelina Mabula amewapongeza Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam ambao wamebuni mradi huo wa kimkakati wenye mafanikio chanya kwa wananchi na hivyo kumuahidi Waziri Mkuu kusimamia mradi huo ili uweze kukamilika kwa wakati.

"Sisi kama Wizara ambao tunasimamia kile ambacho unaelekeza na tutawasimamia National Housing kufanya ile kazi ambayo utakua unaelekeza kwani mradi huu wa kimkakati utakapokamilika vijana watapata ajira  na kukuza uchumi pia." Amesema Mhe. Mabula.

Akitoa taarifa ya mradi huo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam  Ndug.Jumanne Shauri ameeleza kuwa machinjio ya vingunguti yamefikia asilimia 95 za utekelezaji na yamegharimu takribani Shilingi Bilioni 12.49 mpaka kukamilika kwake na hivyo amemuahidi Waziri Mkuu kuwa hadi kufikia Juni 30, 2021 mradi huo utaanza kutumika rasmi ambapo utawanufaisha wananchi wengi na pato la Halmashauri litaongezeka.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.