• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Urejelezaji wa Taka Ngumu

Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam inatambua ongezeko la aina tofauti za taka ngumu zikiwemo za taka za majumbani, taka za viwandani na taka za Hospitali ambazo hutupwa maeneo mbalimbali na hivyo kuweza kusababisha uchafuzi wa mazingira (hewa, maji na Ardhi).

Jiji la Dar es Salaam linakadiriwa kuzalisha zaidi ya tani 4,600 za taka kwa siku. Kati ya hizo ni asilimia 45 hadi 50 tu zinazopokelewa katika dampo sawa na tani 1,200 – 2,000 ya taka zinazokisiwa kuzalishwa kwa siku ambapo taka zinazobaki huishia kwenye maeneo ya wazi, mitaro ya maji, barabara na makazi.

Hali ya usafi wa Jiji la Dar es Salaam hususani udhibiti taka ngumu ni tatizo la muda mrefu ambalo lina changamoto nyingi. Tabia iliyozoeleka miongoni mwa jamii ya utupaji ovyo wa taka katika maeneo yasiyostahili imechangia Jiji kuwa chafu. Kuzagaa kwa taka kunaweza kuwa kichocheo cha milipuko ya magonjwa kama vile kipindupindu na magonjwa mengine ya kuhara na kutapika. Hali ya uchafu Jijini inachangiwa pia na elimu ndogo juu ya usafi wa mazingira, kutotii sheria zilizopo kwa upande wa wananchi na usimamizi hafifu wa sheria za usafi wa mazingira.

Ili kupunguza uchafuzi wa mazingira, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imeandaa sera ya urejelezaji wa taka ngumu ambayo itakuwa ni msingi muhimu kwa Taasisi za Serikali kuanza kutambua na kurasimisha sekta ya urejelezaji taka ambayo awali ilikuwa ikiendeshwa na Taasisi binafsi na vikundi visivyokuwa rasmi.

Katika kuhakikisha hilo linafanyika Halmashauri ya Jiji la Dar Es Salaam inalenga kufanya yafuatayo;

  1. Kubuni miradi mbalimbali ndani ya Jiji itakayohusisha wadau mbalimbali inayolenga urejelezaji taka pamoja na masoko ya uhakika ya taka zilizorejelezwa au bidhaa zilizotokana na taka rejea.
  2. Kuhamasisha jamii juu ya umuhimu wa kurejeleza taka ikiwa ni pamoja na kushirikiana na Halmashauri za Manispaa katika kuhakikisha utenganishaji wa taka unafanyika kuanzia ngazi za uzalishaji (sorting at source).
  3. Kuwatambua na kuwaunganisha wadau mbalimbali wanaojihusisha na teknolojia za urejelezaji taka ndani ya Jiji la Dar es Salaam
  4. Kutenga maeneo ya Viwanda vidogovidogo au karakana (recycling facility) ndani ya dampo au katika maeneo yake ambayo yatafaa kwa kazi zinazohusiana na urejelezaji taka.
  5. Kuhamasisha teknolojia zinazolenga uzalishaji na utumiaji wa bidhaa zitokanazo na taka rejea.
  6. Kuhakikisha inaweka mazingira bora yatakayowezesha ukuaji wa sekta ya urejelezaji taka ngumu kwa kuongeza viwanda na ubora wa bidhaa zake ili ziweze kupata soko ndani na nje ya nchi na hatimaye kukuza pato jamii na Taifa.
  7. Kuwezesha wananchi wa maisha ya chini wakiwemo vijana na wanawake kushiriki katika ubunifu na utumiaji wa teknolojia za urejelezaji taka na hatimaye kuweza kuboresha usafi.

Urejelezaji wa taka una faida nyingi miongoni mwa jamii kama; kuongeza thamani ya taka na kipato katika jamii, kupunguza malundo ya taka katika mitaa na maeneo ya jamii, kupunguza gharama za uendeshaji wa dampo, kupunguza gharama za udhibiti taka katika Manispaa na kuongeza uelewa wa jamii katika uchambuzi wa taka kuanzia ngazi ya kaya.

Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam inalenga kuhakikisha kiwango cha juu cha uzuiaji wa uchafuzi wa mazingira kwa kuweka taratibu zitakazowezesha aina nyingi za taka zinatakazozalishwa katika Jiji ziweze kurejelezwa (Recycling and Re-use) ili kuwa na Jiji safi.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.