• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

Jiji la DSM lapitisha Mapendekezo ya Mpango na Bajeti ya Tshs. Bilioni 278 kwa mwaka 2024/25

Posted on: February 20th, 2024

BARAZA la Madiwani Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, leo Tarehe 20 Februari, 2024 limefanya Mkutano Maalum wa Mapitio ya Mpango na Bajeti ya Mwaka 2023/2024 kwa kipindi cha nusu mwaka (Julai-Desemba, 2023) na kufanya Makadirio ya Mpango na Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2023/2024 wenye Jumla ya Tshs. Bilioni 278, ambapo kati ya fedha hizo kiasi cha Tshs. Bilioni 130 sawa na 47% ya Bajeti yote ni makusanyo kutoka vyanzo vya mapato ya ndani ya Halmashauri na Shilingi Bilioni 148 sawa na 53% ya Bajeti ni fedha za Ruzuku kutoka Serikali Kuu.

Aidha, kikao hicho kilichofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa Arnatouglou na kuongozwa na Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mhe. Omary Kumbilamoto, kilipokea, kikajadili na kisha kupitisha Rasimu ya Mpango na Bajeti ya mwaka wa fedha 2024/2025 ambapo Bajeti hiyo imekua na ongezeko la jumla ya Tshs. Bilioni 40.9 sawa na 46% kutoka katika mapato ya ndani ikilinganishwa na bajeti ya mwaka 2023/24, hii imetokana na mikakati bora iliyowekwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwenye ukusanyaji wa mapato na uibuaji wa vyanzo vipya vya mapato.

Katika Makadirio ya Mpango na Bajeti ya mwaka 2024/2025 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imeweka vipaumbele vitano (05) vitakavyolenga kutatua changamoto kwa ustawi wa wananchi wa Jiji la Dar es Salaam

Akisoma taarifa kuhusu makadirio ya mpango na bajeti ya mwaka 2024/2025 mbele ya Baraza la Madiwani, kwa niaba ya Mkurugenzi wa Jiji, Bw. Julius Ndele alisema "Kwa mwaka wa fedha 2024/2025 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imepanga kukusanya Shilingi Bilioni 130 kutoka kwenye vyanzo vyake vya ndani."


Matumizi ya Mapato ya ndani ya Halmashauri kwa mwaka 2024/2025

Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa mwaka wa fedha 2024/2025 kwenye mapato yake ya ndani inatarajia kutumia fedha kiasi cha Tshs. Bilioni 130 katika mchanganuo ufuatao; Matumizi ya kawaida Tshs. Bilioni 21.3 sawa na 16.3%% ya Bajeti, Miradi ya Maendeleo Tshs. Bilioni 74.4 sawa na 57.2% ya Bajeti, Mishahara Tshs. Bilioni 2.2 sawa na 1.6% na Vyanzo Fungiwa Tshs. Bilioni 31.9 sawa na 24.5% ya mapato ya ndani.

Ruzuku ya Tshs. Bilioni 148 kutoka Serikali Kuu imegawanywa katika maeneo mawili ambayo ni Matumizi ya Kawaida na Miradi ya Maendeleo


Mchanganuo wa Matumizi ya kawaida kwa fedha ya Ruzuku

Kwa mwaka wa fedha 2024/2025 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam inatarajia kutumia Tshs. Bilioni 122.4 ya fedha ya ruzuku sawa na 82.4% kulipa Mishahara na Tshs. Bilioni 1.2 sawa na 0.85% kwa ajili ya Matumizi Mengineyo


Mchanganuo wa Fedha za Miradi ya Maendeleo kwa fedha ya Ruzuku

Katika kipindi kijacho cha 2024/2025 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imepanga kutumia Tshs. Bilioni 24.3 kutekeleza Miradi ya Maendeleo ambayo ni sawa na 16.4%.

Katika kuandaa Rasimu ya Mpango na Bajeti ya mwaka wa fedha 2024/2025 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imeandaliwa kwa kufuata na kuzingatia Sheria ya Bajeti namba 11 ya mwaka 2015, mwongozo wa maandalizi ya bajeti (PBG) ya mwaka 2024/25, Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020-2025, Mpango mkakati wa Halmashauri (SP), Mpango wa maendeleo wa miaka mitano (5YDP III 2020/2021 – 2025/2026), Malengo ya maendeleo endelevu (SDGs), Waraka wa Hazina namba 4 wa mwaka 2024 pamoja na maelekezo mahsusi ya viongozi mbalimbali wa Serikali katika Halmashauri yetu kwa nyakati tofauti.

















Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.