• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

Jiji la DSM latoa mafunzo kwa Watumishi wanaotaraji kustaafu

Posted on: February 8th, 2023

Halmashauri ya Jijj la Dar es Salaam kupitia Idara ya Utawala na Utumishi leo Februari 8,2023 wameandaa Semina na kutoa Mafunzo kwa watumishi wanaokaribia kustaafu hivi karibuni, Mafunzo hayo yaliyofanyika katika Ukumbi wa Karimjee Jijini Dar es Salaam yaliwajumuisha Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Afis Utumishi wa Jiji la Dar es Salaam, Watumishi ambao ni wakufunzi kutoka chuo cha Utumishi wa Umma, watumishi kutoka mfuko wa hifadhi ya jamii 'PSSF' pamoja na watumishi kutoka bank ya CRDB.

Akifungua mafunzo hayo Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es-Salaam Bi. Tabu Shaibu amesema, baadhi ya watumishi wamekuwa wanahangaika na kulalama kwa changamoto ya ugumu wa maisha mara baada ya muda wao wa utumishi kuisha na kurudi uraiani kuanza maisha mengine nje na kazi ya utumishi wa Umma, ambapo waliowengi hushindwa kuwa na mipango madhubuti ya baadaye.

Akiendelea kuongea katika mafunzo hayo Bi. Tabu Shaibu ameeleza kuwa, kila mtumishi anawajibu wa kuonesha mchango wake mkubwa muda wote hata baada kutoka kazini, jambo linalotoa taswira nzuri na kuonesha mchango mkubwa kwa jamii, kufanya hivyo kutasababisha kuepuka changamoto zinazoweza kujitokeza wakati wa kustaafu "Tunachokitaka ni kuwa na mchango mkubwa wa wastaafu katika Halmashauri yetu kwani wengi wanaonekana kuogopa kuanza maisha ya uraiani hivyo ni matumaini yangu mafunzo haya yatakua ni njia ya mafanikio kwa watumishi hao wanaoelekea kustaafu"

Aidha, kwa upande wake Afisa utumishi wa Halmashauri ya Jiji la Dares-Salaam, Bi. Benadeta Mwaikambo amebainisha jumla ya watumishi 91 wanatarajia kustaafu kuanzia mwezi Januari mpaka mwezi Desemba mwaka huu akiongeza kuwa kushindwa kuanzisha miradi ya kujikimu kwa watumishi wanapostaafu kuwa ni changamoto kubwa inayowakabili waliowengi baada ya utumishi wao hivyo ofisi ya utumishi ikaamua kuanziisha mafunzo ya kuwaweka tayari wastaafu hao pindi wanapomaliza kuutumikia Umma nakuona maisha mengine kama maisha ya Utumishi.

“Sisi kama Ofisi ya Utumishi tumeona ni vyema kuanzisha mafunzo haya kwani tumebaini kuwa watumishi wengi wa Umma pindi wanapostaafu wanakosa muelekeo wa maisha kwa kuwa walishazoea maisha ya Utumishi hivyo ni katumaini yangu kwamba mafunzo haya yatawapa mwanga wa kuweza kupambana baada ya maisha ya Utumishi wa Umma hii ndo sababu tumewaletea wakufunzi kutoka chuo cha Utumishi wa Umma pamoja na watumishi kutoka mfuko wa hifadhi ya jamii PSSF ili waweze kupata elimu itakao wafanya wajiandae vyema na maisha ya ustaafu na kuyaona ni kama maisha ya Utumishi wa Umma.”

Sambamba na hilo Bi. Mwaikambo ameeleza kuwa zoezi hili lililoanza la utoaji wa mafunzo ni endelevu na kila mwaka watakua wanafanya mafunzo hayo ya kuwaandaa wastaafu kukabiliana na changamoto zitakazowakabili pindi wanapomaliza majukumu yao ya kuutumikia Umma.

Akitoa Shukrani zake kwa Ofisi ya Utumishi kwa niaba ya Watumishi wengine wanaotarajia kustaafu hivi karibuni Bwana Nashon ameeleza kuwa Sisi kama watumishi tunaotarajia kuataafu tumejiandaa vyema kupokea mafunzo haya na tunawahakikishia yote tutakayoelekezwa tutayafuata na kuyafanyia kazi ili yaweze kutuongoza baada ya maisha ya kuutumikia Umma.

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.