• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

Kamati ya Kudhibiti UKIMWI Halmashauri ya Jiji la DSM yapata mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kupambana na maambukizi ya UKIMWI

Posted on: May 2nd, 2023

Katika kutekeleza sera ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kupitia Idara ya Maendeleo ya Jamii Leo Mei 02, 2023 wametoa mafunzo kwa Kamati ya kudhibiti VVU/UKIMWI ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam lengo likiwa ni kuwajengea uwezo wa namna ya kudhibiti maambukizi ya ugonjwa wa UKIMWI katika Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam.

Mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Arnatouglou uliopo Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam yaliweza kuhudhuriwa na madiwani ambao ni wajumbe wa Kamati ya kudhibiti UKIMWI Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ikiongozwa na Naibu Meya wa Jiji, Maafisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam pamoja na viongozi wote wa baraza la watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI (KONGA).

Akifungua Mafunzo hayo Naibu Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Mhe. Ojambi Masaburi ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya kudhibiti UKIMWI amesema “Ni matumaini yangu mafunzo Haya yatawajengea ninyi Kama Kamati ya kudhibiti UKIMWI uwezo juu ya namna ya kudhibiti UKIMWI katika Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwani Nina Imani mtashirikiana na wadau mbalimbali katika kupambana na ugonjwa huo hatarishi na hatimaye kufikia malengo mliyojiwekea.”

Akiwezesha mafunzo hayo maratibu wa VVU/UKIMWI Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam (CHAC) Ndg. Barnabas Kisai ameeleza kuwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wameendelea kutekeleza afua mbalimbali za kudhibiti VVU na UKIMWI kwani Halmashauri kupitia mapato ya ndani imekua ikitenga fedha kiasi cha shilingi milioni 150 kwaajili ya kuhakikisha Jamii inahamashwa zaidi juu ya namna ya kujikinga na ugonjwa wa UKIMWI na pia kuhakikisha wale wote walioadhirika na ugonjwa huo kujitokeza kwa wingi ili kuweza kupata huduma kwa karibu zaidi.

Aidha Ndg. Kisai aliweza kutoa maelezo jumla ya uratibu wa shughuli za VVU/UKIMWI katika Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam huku akiwakumbusha Wajumbe wa Kamati ya kudhibiti UKIMWI wajibu na majukumu yao katika kuhakikisha wana tekeleza afua mbalimbali za kudhibiti ugonjwa wa UKIMWI na pia kuendelea kutoa elimu kwa Wananchi wa Kata zao juu ya namna ya kudhibiti ugonjwa wa UKIMWI. “Japo tunawakumbusha majukumu yenu lakini pia tunawashukuru sana Madiwai wa Kamati yetu ya kudhibiti UKIMWI kwa kupambana kuhakikisha Kamati inaendelea na utekelezaji wa afua mbalimbali za VVU na UKIMWI katika Halmashauri yetu." Ameeleza Ndg. Kisai

Naye Mratibu wa kudhibiti VVU/UKIMWI Sekta ya Afya  Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Dkt. Aisha Zuheri (DACC) ameeleza kuwa “Idadi kubwa ya waadhirika wa ugonjwa wa UKIMWI ni vijana wa kike kuanzia umri wa miaka 15 hadi 24 lakini kutoka na jitihada za kutoa elimu Mara kwa mara katika Kliniki zetu tumeweza kufikia asilimia 102.8 ya kufubaza virusi vya UKIMWI katika Halmashauri yetu.”

Sambamba na hilo Dkt. Aisha ameweza kutoa tofauti kati ya VVU na UKIMWI ambapo ameeleza kuwa VVU ni vimelea vidogo ambayo havionrkani kwa macho huku UKIMWI ikiwa ni mkusanyiko wa magonjwa yanayotokana na kudhoofika kwa nguvu za mwili kujikinga na maradhi hivyo sio kila mwenye VVU ana UKIMWI.

Kwa upande wake mwenyekiti wa baraza la watu wanahis hi na VVU/UKIMWI (KONGA) Bw. Emmanuel Robert Msinga amesema “Napenda kutoa shukrani zangu kwa madiwani wa Kamati ya kudhibiti UKIMWI pamoja na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kupitia Idara ya Maendeleo ya Jamii kwani wamekua na mchango mkubwa sana katika kuhakikisha sisi kama KONGA tunapambana zaidi hadi tumeweza kuanzisha mashamba mbalimbali pamoja na mifugo mbalimbali hii inadhihirisha kuwa sio kila mwathirika wa Ugonjwa wa UKIMWI hawezi kufanya kazi hivyo niwaombe vijana wengine pamoja na watu wengine wenye maambukizi ya ugonjwa wa Uko wasisite kujitokeza na kuungana nasi bila kuogopa kwani sio kila aliyepata maambukizi ndo mwisho wa maisha.”

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.