• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Historia ya Jiji

Utangulizi

Jiji la Dar es Salaam lipo kati ya Latitudo nyuzi 6 hadi 7 na Longitudo kati 39.45 kwa upande wa Mashariki na nyuzi 39 kwa upande wa Magharibi, Kusini mwa Ikweta na upande wa Magharibi, Kusini na Kaskazini. Jiji linapakana na Mkoa wa Pwani, upande wa Mashariki linapakana na Bahari ya Hindi, ambapo kuna ufukwe wenye urefu wa km. 124 unaoanzia Pemba Mnazi hadi Mbweni.

Jiji la Dar es Salaam lina eneo la ukubwa wa kilomita za Mraba zipatazo 1,800; kati ya hizo, kilomita za mraba 1,350 ni eneo la nchi kavu ikijumuisha visiwa vinane vilivyopo katika eneo la bahari ya Hindi na kilomita za mraba 450 ni eneo la maji ya bahari. Eneo la Jiji la Dar es Salaam ni sawa na asilimia 0.2 ya eneo la nchi nzima ambalo ni kilomita za mraba 881,289.

Hali ya Hewa

Jiji hili lina hali ya hewa ya Joto ya Pwani ya Tropical, likiwa na wastani wa nyuzi joto 25 hadi 33 sentigredi na wastani wa mvua wa mililita 1,000 katika misimu miwili ya vuli ambayo ni miezi ya Oktoba – Desemba na Masika ambayo huanza miezi ya Machi – Mei. Wakati mwingi Jiji hutawaliwa na pepo zivumazo toka baharini zikitokea Kusini, Mashariki na Kaskazini mwa Bahari ya Hindi.


Idadi ya watu

Kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2012 Jiji lina idadi ya watu 4,364,541, ambapo kati yao wanaume ni 2,125,786 na wanawake ni 2,238,755. Aidha, idadi ya watu imekua ikiongezeka kwa wastani wa asilimia 5.6 kwa mwaka. Wastani wa watu kwa kila kilomita moja ya mraba ilikuwa ni 3,137 na ukubwa wa Kaya ni wastani wa watu 4 kwa Kaya. Kwa ongezeko hilo la watu kwa mwaka, Jiji la Dar es Salaam mwaka 2018 linakadiriwa kuwa na idadi ya watu 6,107,473. Idadi hii ya watu inaongeza msongamano wa watu wanaokadiriwa kuwa 4,383 kwa kila kilometa moja ya mraba.


Historia ya Halmashauri ya Jiji

Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imekuwa inaliongoza Jiji kutoka mwaka 1961 mpaka mwaka 1972, ambapo Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilizivunja Halmashauri zote nchini na kuwa chini ya Usimamizi wa Serikali Kuu (Madaraka Mikoani)

Serikali Kuu ilizirudisha Serikali za Mitaa Nchini, Chini ya Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji) na. 8 ya mwaka 1982, ambapo Halmashauri ya Jiji ilianza kutekeleza majukumu yake ya kutoa huduma kwa wananchi kuanzia mwaka 1983.

Mwaka 1996 Serikali Kuu iliivunja Halmashauri ya Jiji na kuunda Tume ya Jiji la Dar es Salaam, kwa Tangazo la Serikali Na. 110 na 111 ya tarehe 28 Juni mwaka 1996.

Tume ya Jiji ilifanya kazi kwa kipindi cha miaka minne, ambapo mwaka 2000 Serikali iliunda mamlaka nne za Serikali za Mitaa za Mkoa wa Dar es Salaam kwa sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji) Na. 8 ya Mwaka 1982, kama ilivyo rekebishwa kwa sheria na. 6 ya mwaka 1999.


Utawala

Kiutawala Jiji limegawanyika katika Halmashauri sita za Serikali za mitaa ambazo ni:

  • Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam
  • Halmashauri ya Manispaa ya Temeke
  • Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni
  • Halmashauri ya Manispaa ya Ilala
  • Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo na
  • Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni

Muundo

Halmashauri ya Jiji inaundwa na Baraza la Madiwani, Idara tano na Vitengo vinne.


Baraza la Madiwani

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam linaundwa na Madiwani 26 kutoka katika Manispaa tano za Jiji la Dar es Salaam na linawakilishwa na Wajumbe wafuatao: Mameya 5, Madiwani 16 na Wabunge 5.

Mstahiki Meya wa Jiji ni Kiongozi Mkuu na Mkurugenzi wa Jiji ni Mtendaji Mkuu kwa upande wa Serikali za Mitaa. 


Majukumu ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam
Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam iliundwa na kupewa majukumu ya kuratibu na kusimamia shughuli za uendelezaji wa Jiji katika Halmashauri za Manispaa zote tatu. Majukumu hayo ni kwa mujibu wa Sheria za serikali za mitaa (Mamlaka za Miji) Na.8 ya mwaka 1982 kifungu cha 69A kama ilivyorekebishwa na sheria Na.6 ya mwaka 1999.

Majukumu hayo ni kama ifuatavyo:

  • Kuratibu Mamlaka na wajibu wa kila Halmashauri za Manispaa juu ya miundombinu na matumizi bora ya ardhi.
  • Kuandaa Mpango Mkakati kwa ajili yakuhakikisha kuwa panakuwepo na maendeleo endelevu ya Jiji
  • Kukuza ushirikiano kati ya Mamlaka za Halmashauri zote zilizopo katika Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam.
  • Kushughulikia masula yote yanayohusu ushirikiano kati ya Malmaka za Serikali za Mitaa zilizopo katika Jiji la Dar es Salaam.
  • Kuhakikisha panakuwepo amani na utulivu pamoja na kutoa msaada katika huduma kama vile Zimamaoto na maokozi, Polisi na magari ya kubeba wagonjwa.
  • Kutekeleza majukumu mengine yoyote kama itakavyokubalika na Halmashauri nyingine zilizopo.
  • Kutekeleza majukumu ya itifaki na sherehe za Kimkoa au /na Kitaifa.

Uboreshaji wa Muundo wa Jiji la Dar es Salaam kuwa mamlaka sita umeleta ufanisi mkubwa katika utoaji bora wa huduma kwa jamii kwani madaraka yamesogezwa karibu zaidi na wananchi.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.