• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

DC Ilala Awataka Wananchi kuweka Jiji Katika Hali ya Usafi

Posted on: February 25th, 2023

Katika kuendeleza na kutekeleza kampeni ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe.Amos Makaka Mkuu wa Wilaya ya Ilala Leo Februari 25,2023 ameshiriki zoezi la usafi katika Kata ya Kariakoo ambapo usafi huo ulijumuisha maeneo ya Barabara ya Bibi Titi, Barabara ya Nkurumah pamoja na maeneo ya barabara ya Lumumba na Barabara ya Morogoro.

Zoezi hilo lililoongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Mpogolo akiambatana na Katibu Tawala wa Wilaya ya Ilala, Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Diwani wa Kata ya Gerezani na Jangwani, Watumishi kutoka Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Watendaji wa Mtaa, viongozi wa Chama cha Mapinduzi wa Kariakoo Mashariki, viongozi kutoka shujaa wa maendeleo na Ustawi wa Jamii Tanzania (SMAUJATA), wadau kutoka Bank ya CRDB na wadau mbali mbali wa usafi wakiwemo Wejisa Company limited, Kajenjere Trading Company Limited, Sateki Trading Limited, Umoja wa Madereva wa Pikipiki Mjini Kati, Vingunguti na Msimbazi Jogging Club pamoja na Wananchi wa Kata ya Kariakoo.

Aidha, Mhe.Edward Mpogolo amewashukuru viongozi wa Machinga na Bodaboda kwa kuweza Kuhudumu katika Barabara ya Lumumba hivyo ameelekeza Vigingi na Miti kutoka barabara ya Airport vihamishwe na kuletwa barabara ya Lumumba ili kuboresha eneo hili.

“Kutokana na ukubwa wa Barabara ya Lumumba napenda kuwaomba watu wa maduka waboreshe maeneo yao huku upande wa katikati ya barabara tutahakikisha Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam tunashirikiana na Wamachinga, Bodaboda pamoja na wadau mbalimbali ili kuhakikisha barabara hii inakuaje safi na bora kwani Dar es Salaam hususani Wilaya ya Ilala kwani ndiyo Kitovu cha kupokea wageni wanaoingia Nchini.”

Sambamba na hilo Mhe. Mpogolo amemuelekeza Mkurugenzi wa Jiji kwa kushirikiana na watendaji wake kuhakikisha wanaandaa barua na Kuwapelekea wafanyabiashara wote wenye Majengo kuanzia barabara ya Airport hadi Ikulu ili kuona namna gani watawaelekeza kuboresha mazingira na miti gani waweze kupanda kwenye maeneo yao ili kuboresha mazingira ya Mji wetu.

Aidha Mhe. Mpogolo amewataka vijana wote wanaobandika stika maeneo ya Lumumba kuhakikisha wanaweka Jiji safi baada ya kumaliza kazi zao. Akiendelea kuongea katika zoezi Hilo Mhe.Mpogolo ameelekeza vifusi vyote vya mchanga vilivyopo barabarani kuondolewa pia watu wa ustawi wa jamii watafute namna ya kuwaelekeza watu wote wanaolala kando ya barabara na ndani ya Viwanja wahakikishe wanawaondoa katika maeneo hayo kwa kutumia utaratibu maalumu huku akiwataka wanaoegesha magari maeneo ambayo sio ya maegesho kupigwa faini kwani ni moja ya uchafuzi wa mazingira.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam Eng. Amani Mafuru ameeleza kuwa kampeni hii ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam imekua ya mafanikio zaidi kwa Jiji la Dar es Salaam kuwa Safi kwani wananchi wameonekana kujitokeza kwa wingi katika zoezi la usafi.

“Nipende kutoa Shukrani zangu za dhati kwa Mkuu wa Mkoa Wa Dar es Salaam Mhe.Amos Makalla kwa kuanzisha Kampeni hii ambayo ni endelevu kwani kutoka na kampeni hii Mkoa wa Dar es Salaam umeweza kushika nafasi ya Sita barani Afrika kwa usafi hivyo niwaombe wananchi kuhakikisha usafi ni Sehemu ya maisha yetu ya Kila siku na si mpaka tusubiri usafi wa mwisho wa mwezi.” Ameeleza Eng. Mafuru.

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.