• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

DC Mpogolo awataka wafanyabiashara kuwa wazalendo

Posted on: June 13th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Mpogolo amewataka Wafanyabiashara wa Kariakoo kuwa wazalendo kwa kuhakikisha wanashirikiana na Serikali kuwapanga wafanyabiashara ndogondogo (machinga) katika maeneo sahihi bila kuzuia biashara nyingine na njia za watembea kwa mguu pamoja na kuwatambua wafanyabiashara wote ambao sio machinga ila wameweka meza kama machinga kwa lengo la kukwepa kodi.

Mhe. Mpogolo ametoa maagizo hayo leo Juni 13, 2024 wakati wa kikao kazi na Jumuiya ya Wafanyabiashara Kariakoo kilichofanyika a katika ukumbi wa Arnatouglou Jijini Dar es Salaam kilicholenga kuwasilisha kero za wafanyabiashara hao.

Akiongea na Wafanyabiashara hao Mhe Mpogolo amesema “Kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam nina wajibu wa kusimamia na kushiriki katika kutatua changamoto zenu zinazowakabili kwani changamoto zote nimezichukua na nitakwenda kuzisimamia ziweze kutekelezwa kwa wakati zaidi hivyo niwaombe muwe watulivu kwani Serikali yetu iliyoko Chini ya Rais wetu Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ni sikivu na inawajali wafanyabiashara itahakikisha changamoto hizi zinatatuliwa kwani tumeanza kuweka taa baadhi ya maeneo ili kuhakikisha biashara zinafanyika masaa 24. Pia, niwaombe Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuendelea kutoa elimu ya kodi kwa wafanyabiashara ili kutengeneza ufahamu kwa wafanyabiashara lakini pia niwatake Jeshi la Polisi wafuate maelekezo ya Waziri Mkuu ambayo aliyatoa juu ya kamatakamata”.

Sambamba na hilo, Mhe. Mpogolo amewapongeza Wafanyabiashara kwa kuwa walipa kodi wazuri kwa Serikali huku akiwataka kuendelea na vikao vya mara kwa mara ambavyo vitakua na matokeo chanya ya kujenga pamoja na kukumbushana yote yanayosahaulika bila kusahau kukumbushana kujisajili.

Awali wakiwasilisha kero kwa Mhe. Mpogolo, wafanyabiashara wa Kariakoo wameeleza kuwa wafanyabiashara ndogondogo (wamachinga) ni lango la kutorosha mapato ya serikali, kwa kuwa kuna wafanyabiashara wakubwa Karikaoo ambao wamekuwa wakifunga maduka na kusambaza mizigo yao kupitia wamachinga huku wakionyesha kutoridhishwa na namna Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inavyowatendea hasa kwenye ushuru.

Akitoa Shukrani zake kwa Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Kariakoo Ndg. Martin Mbwana amesema “Nipende Kukushukuru Mkuu wa Wilaya kwa kuitikia wito wetu na kuja kuongea na sisi ila ningeshauri kwamba hatua madhubuti zinapaswa kuchukuliwa ili kukabiliana na hali ya wamachinga ambao wamekua wakikwepa kodi."

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.