• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

Jaffo azindua mpango wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam wa kukuza na kuendeleza utalii

Posted on: March 17th, 2018

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Suleimani Jaffo (Mb), leo tarehe 17 Machi, 2018 amekua mgeni rasmi katika uzinduzi wa shughuli za kukuza na kuutangaza utalii katika Jiji la Dar es Salaam. 

Akizingumza katika hafla hiyo iliyohudhuriwa na viongozi wa Serikali katika ngazi ya Mkoa, Waheshimiwa Madiwani, wadau mbalimbali katika sekta ya utalii na vikundi vya wajasiriamali vinavyoshughulika katika biashara ya utalii katika Jiji la Dar es Salaam, Waziri Jaffo ametoa pongezi kwa Halmashauri ya Jiji Dar es Salaam kwa jitihada inazozifanya za  kukuza na kutangaza utalii nchini.

Aidha, ameziasa Mamlaka za Serikali za Mitaa kote nchini kuiga jitihada zinazofanywa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam katika kukuza na kuendeleza utalii nchini.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul C. Makonda amepongeza jitihada zinazofanywa na Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji linaloongozwa na Mstahiki Meya wa Jiji pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji Dar es Salaam katika kukuza na kuendeleza utalii jijini pamoja na kuunga mkono jitihada za Serikali ya Awamu ya Tano katika kuwaletea Watanzania maendeleo.

Mhe. Paul Makonda amepiga marufuku baadhi ya watendaji Serikalini wanaozuia wasanii kurekodi video za nyimbo na sinema zao kwenye mandhari (location) mbalimbali za Jiji la Dar es Salaam kwani kwa kufanya hivyo inarudisha nyuma fursa za kutangaza na kukuza utalii wa Jiji la Dar es Salaam kupitia kazi za sanaa za wasanii hao.

Nae, Mstahiki Meya wa Jiji, Mhe. isaya Mwita Charles amesema Jiji la Dar es Salaam litashirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii, Chuo cha Taifa cha Utalii na wadau mbalimbali wa utalii ili kuhakikisha vivutio vingi vya utalii vinavyohusu historia ya nchi hii, mila, desturi na utamaduni, majengo ya kihistoria, siasa, uchumi na mambo ya jamii vinatangazwa ili kukuza utalii katika Jiji la Dar es Salaam na kuweza kutunza mazingira, kutoa ajira kwa wananchi wetu na pia kuchangia pato la Taifa.

Awali akiwasilisha taarifa ya mpango wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam katika kuendeleza utalii jijini Dar es Salaam kwa Waziri Jaffo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Bi. Sipora Liana ameeleza jitihada mbalimbali zilizofanywa na Halmashauri ikiwa ni pamoja na ununuzi wa mabasi ya kubeba watalii, uwekaji wa nembo malum katika majengo ya kihistoria, kuanzisha Kitabu cha Utalii kinachotoa taarifa mbalimbali ya vivutio, mahali pa kwenda, vitu muhimu vya kuangalia na taarifa za kiusalama ili kumrahisishia mgeni anapotembelea sehemu mbalimbali jijini pamoja na kutoa mafunzo kwa waongoza utalii (Tour Guides) watakaotumika kuongoza wageni na watalii watakaotoa taarifa sahihi za vivutio, historia ya Mji wakati wa kuwatembeza watalii kwenye vivutio mbalimbali.

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.