• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

Jiji la Dar es Salaam lavuka lengo katika utoaji wa Chanjo ya Polio

Posted on: May 26th, 2022

Chanjo ya polio ni chanjo ambayo inatolewa kwa ajili ya kujikinga na virusi vya polio. Virusi hivi ni kati ya virusi ambavyo vinaleta ugonjwa wa kupooza, hivyo kusababisha mtu kushindwa kutembea, kuendelea na shughuli zake za kila siku na huathiri zaidi watoto walio na umri wa chini ya miaka mitano.

Nchini Tanzania Serikali kupitia Wizara ya Afya iliendesha kampeni ya chanjo ya polio kwa watoto walio na umri wa chini ya miaka mitano. Kampeni hiyo ilianza tarehe 18 Mei hadi 21 Mei, 2022.

Kampeni hii ilifanyika hapa nchini kutokana na maelekezo ya Shirika la Afya Duniani baada ya kubainika kuwepo kwa virusi vya polio nchini Malawi na kufanya mataifa ya jirani na  nchi hiyo ikiwemo Tanzania kupata chanjo ya kujikinga dhidi ya ugonjwa huo.

Katika Jiji la Dar es Salaam, Mganga Mkuu wa Jiji la Dar es Salaam, Dr. Elizabeth Nyema, ametoa tathimini ya zoezi zima la utoaji wa chanjo na kusema kuwa katika kipindi cha siku nne za kampeni ya utoaji wa chanjo hiyo walitarajia kutoa chanjo kwa jumla ya watoto 221,201.

Alisema kuwa hadi kampeni hiyo ilipomalizika walifanikiwa kutoa chanjo kwa jumla ya watoto 266,908 ambayo ni sawa na asilimia 121. Hivyo kwa upande wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imefanikiwa kwa kiasi kikubwa katika zoezi hilo kwani muitikio wa wananchi ulikuwa ni mkubwa.

Dr. Nyema alisema kuwa hata baada ya kumalizika kwa siku nne za kampeni hiyo bado kuna baadhi ya wananchi waliojitokeza kuomba wapate chanjo hiyo kwa kuwa hawakufanikiwa kufikiwa na watoa huduma katika siku zile nne za kampeni. Kutokana na sababu hii Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam iliendelea kutoa chanjo hiyo kupitia vituo vyake vyote vya afya.

Dr. Nyema alisema kuwa wanawakinga watoto walio na umri wa chini ya miaka mitano kwa sababu katika umri huo huwa hawana kinga za kutosha ukilinganisha na wale wenye umri zaidi ya huo.  Chanjo hiyo husaidia kuwakinga watoto wa rika hiyo ili wasipate maambukizi ya magonjwa mbalimbali ikiwemo ugonjwa wa polio.

Aidha, amewahakikishia wananchi wa Jji la Dar es Salaam kuwa chanjo zote zinazotangazwa na kutolewa na Serikali zimefanyiwa utafiti wa kina na ziko salama. Amewataka wananchi kujitokeza kupata chanjo hizo kwa wakati kwa ajili ya kujikinga na magonjwa mbalimbali hasa magonjwa ya mlipuko.

Dr. Nyema amewapongeza wananchi wote wa Dar es Salaam kwa kuendelea kufuata taratibu za afya na kutoa wito kuwa wahakikishe pale ambapo Serikali inatangaza kampeni mbalimbali waweze kuwa na mwitikio chanya na kujitokeza kwa wingi kwa ajili ya kupata chanjo hizo.

Amesema, “Tumetoka kwenye chanjo ya polio, tunaendelea na chanjo ya UVIKO 19 lakini pia kuna chanjo zile za watoto chini ya miaka mitano zinazoendelea vituoni, wananchi wahakikishe wanawafikisha watoto kupata chanjo hizo ili kuwakinga na magonjwa mbalimbali.”

Kampeni ya utoaji wa chanjo ya polio katika Jiji la Dar es Salaam ilitekelezwa kwa wataalamu wa afya kupita nyumba kwa nyumba, kwenye maeneo ya shule za watoto, masoko, maeneo ya mikusanyiko mikubwa ya watu na kwenye vituo vya kutolea huduma za afya. Hivyo, zoezi la utoaji wa chanjo hii lilifanikiwa kwa kiwango kikubwa kutokana na mwitikio mkubwa wa wananchi.

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • Mwenge wa Uhuru waweka jiwe la Msingi Kituo cha Afya Mzinga

    June 03, 2025
  • Mwenge wa Uhuru wakagua mradi wa vijana "Ulipo Tupo" Tabata

    June 03, 2025
  • Mradi wa Ujenzi wa Barabara ya Magengeni - Chang'ombe umewekewa jiwe la msingi na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa

    June 03, 2025
  • Mwenge wa Uhuru wazindua mradi wa Nishati Safi Soko la Samaki Feri

    June 03, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.